Mhariri 
Mtendaji wa gazeti la Mtanzania, Absalom Kibanda akimfariji mjane wa 
marehemu Mpoki Bukuku, Lilian nyumbani kwa marehemu, Tabata Bwawani, Dar
 es Salaam. Bukuku alifariki juzi baada ya kugongwa na gari Barabara ya 
Bagamoyo karibu na Kituo cha ITV, Mwenge. PICHA NA RICHARD 
MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
                               Kibanda akimfariji mama mzazi wa marehemu Mpoki Bukuku
 Kiongozi
 wa Chama cha ACT, Zitto Kabwe (kulia) akizungumza jambo na Shemeji wa 
marehemu Mpoki Bukuku, Edwin Mjwahuzi alipokwenda kuwafariji wafiwa 
nyumbani kwa marehemu, Tabata Bwawani.
 Zitto Kabwe (kulia) akizungumza na kaka wa Marehemu Mpoki, Gwamaka Bukuku wakati wa msiba huo
 
Waandishi wa habari wakiwa kwenye msiba wa marehemu Mpoki Bukuku ambaye 
alikuwa Mpigapicha mwandamizi wa magazeti ya Kampuni ya The Guardian
                                      Wanahabari wakijadiliana mambo wakati wa msiba huo
Mmiliki 
wa Blogu hii, Kamanda Richard Mwaikenda, ambaye pia ni Mpigapicha Mkuu 
wa gazeti la Jambo Leo, Kamanda Richard Mwaikenda (kulia) akiwa na 
wanahabari wenzie kwenye msiba huo.Kutoka kushoto ni Mpigapicha wa 
Waziri Mkuu, Hilary Bujiku, Mmiliki wa Blog ya K-VIS, Khalfan Said, 
Mmiliki wa Blog ya Michuzi, ambaye pia ni Mpiga Picha na Mwandishi wa 
Habari Msaidizi wa Rais, Muhidini Issa Michuzi, Mpigapicha Mkuu wa 
Gazeti la Mwananchi, ambaye ni shemeji wa marehemu Mpoki, Edwin Mjwahuzi
 na Francis Chirwa ambaye ni mmoja wa viongozi wa Bodi ya Wahariri wa 
Gazeti la Raia Mwema. 
                                                                            Waombolezaji wakiwa kwenye msiba
Jirani rafiki wa karibu wa marehemu, Mpoki, maarufu kwa jina la Mijisu  akilia wakati wa msiba 
 
 
 
 
  
 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni