Kampuni
 ya Magazeti ya Serikali (TSN) Wachapaji wa magazeti ya Daily News, 
Sunday News, Habarileo, Habarileo Jumapili na Spotileo imeadhimisha 
miaka 10 tangu kuanza kwa gazeti la Habarileo mnamo Desemba 21, 2006 kwa
 kukata keki huku Uongozi wa Kampuni hiyo ukitangaza shamra shamra za 
mwezi mmoja wa kusherehekea kuzaliwa kwa gazeti hilo.
Aidha
 ili kushirikiana na wadau wengine, Kampuni imetangaza punguzo la 
asilimia 30 kwa mteja atakeatangaza tangazo lake ndani ya siku 30 za 
shamrashamra katika gazeti la Habarileo. 
 Miongoni
 mwa wageni maalum waliohudhuria sherehe hizo ni Mhariri Mtendaji wa 
zamani wa TSN, Isack Mruma (wapili kulia) ambaye kwa sasa ni Ofisa wa 
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambaye alishiriki kukata keki 
pamoja na Mhariri Mtendaji wa sasa Dk Jim Yonaz (wapili kushoto) na 
Naibu Mharidi Mtendaji, Tuma Abdallah. Kushoto akishuhudia ni Meneja 
Mauzo na Masoko, Januarius Maganga.  
 Naibu Mharidi Mtendaji, Tuma Abdallah akimlisha keki Kaimu Mhariri wa Gazeti la Habarileo, Nicodemus Ikonko. 
 Shangwe za miaka 10 ya Habarileo.
 ME wa zamani wa TSN Isack Mruma akilishwa keki na ME wa TSN Dk Jim 





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni