TSN YAADHIMISHA MIAKA 10 YA GAZETI LAKE LA HABARILEO

 Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Wachapaji wa magazeti ya Daily News, Sunday News, Habarileo, Habarileo Jumapili na Spotileo imeadhimisha miaka 10 tangu kuanza kwa gazeti la Habarileo mnamo Desemba 21, 2006 kwa kukata keki huku Uongozi wa Kampuni hiyo ukitangaza shamra shamra za mwezi mmoja wa kusherehekea kuzaliwa kwa gazeti hilo.
Aidha ili kushirikiana na wadau wengine, Kampuni imetangaza punguzo la asilimia 30 kwa mteja atakeatangaza tangazo lake ndani ya siku 30 za shamrashamra katika gazeti la Habarileo.
 Miongoni mwa wageni maalum waliohudhuria sherehe hizo ni Mhariri Mtendaji wa zamani wa TSN, Isack Mruma (wapili kulia) ambaye kwa sasa ni Ofisa wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambaye alishiriki kukata keki pamoja na Mhariri Mtendaji wa sasa Dk Jim Yonaz (wapili kushoto) na Naibu Mharidi Mtendaji, Tuma Abdallah. Kushoto akishuhudia ni Meneja Mauzo na Masoko, Januarius Maganga. 
 Naibu Mharidi Mtendaji, Tuma Abdallah akimlisha keki Kaimu Mhariri wa Gazeti la Habarileo, Nicodemus Ikonko.
 Shangwe za miaka 10 ya Habarileo.
 ME wa zamani wa TSN Isack Mruma akilishwa keki na ME wa TSN Dk Jim

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni