KIMBUNGA MATTHEW CHAFIKA FOLORIDA NA KUAANZA KUSABABISHA MAAFA


Kimbunga hatari kiitwacho Matthew kimeikumba Florida na kuwaacha watu 200, 000 bila umeme huku mamilioni ya watu wakiwa katika maeneo yatakayopitiwa na kimbunga hicho.

Rais Barack Obama ametangaza hali ya tahadhari katika majimbo ya Florida, Georgia pamoja na South Carolina, kufuatia kimbunga hicho kinachoambatana na mvua.

Wakati huo huo vifo vilivyotokana na kimbunga Matthew nchini Haiti vimeongezeka na kufikia zaidi ya watu 300.
                                   Kimbunga Matthew kikisukuma miti kama inavyoonekana 
                            Watu wakiwa wamevalia makoti ya mvua ya nailoni kujikinga na mvua 
   Mama akiwa na mtoto wake katika kambi maalum salama kwa watu walihamishwa kwenye maeneo yao hatari

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni