Mradi
 mkubwa wa kijiji cha digitali cha Ololosokwan, Loliondo umezinduliwa 
rasmi mwishoni mwa wiki, miaka miwili tangu kutiwa saini kwa uanzishwaji
 wake kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni
 (Unesco) na kampuni ya Samsung.
Hiki
 kitakuwa ni kijiji cha nne cha digitali barani Afrika cha kwanza kikiwa
 nchini Afrika Kusini huku kingine kikiwa Gabon na Ethiopia.
Kijiji
 hicho cha digitali ni nadharia ya Samsung katika kurejesha faida kwa 
umma na kina huduma mbalimbali ambazo zikiunganishwa na haja ya wananchi
 zitasaidia kubadili maisha ya wamasai na kuondokana na utegemezi wa 
mifugo pekee.
Uzinduzi
 rasmi wa kijiji hicho umefanywa na Mkuu wa mkoa Arusha Mrisho Gambo kwa
 niaba yaWaziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto 
Ummy Mwalimu.
Kijiji
 hicho cha digitali kina shule yenye tehama ikiwa na maunganisho ya 
intaneti, kiliniki ya kisasa ikiwa na kituo cha teknolojia ya 
mawasiliano yenye kuwezesha utabibu (telemedicine) na jenereta 
linalotumia nguvu za jua.
Mradi
 huo ambao ulishuhudiwa utiaji saini na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya
 Taifa ya UNESCO, Bi. Leah Kihimbi kutoka Wizara ya Habari, Vijana, 
Utamaduni na Michezo na Dkt. N. Iriya kutoka Shirika la Afya Duniani 
(WHO) Dar es Salaam na wafanyakazi wa UNESCO mwaka 2014, kukamilika 
kwake kunawezesha UNESCO na serikali ya Tanzania kuwapatia wakazi wa 
eneo hilo huduma bora za afya na vijana wa Kimasai nafasi ya kupata 
elimu kutokana na ukweli kuwa kwa utamaduni na kazi zao za ufugaji 
wamekuwa wakipata shida ya kupata elimu.
Utiaji
 saini wake katika mwaka huo ulifanywa na Mkuu wa ofisi na Mwakilishi 
Shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues na Mkurugenzi wa Samsung 
Electronics nchini Tanzania, Bw. Mike Seo .Kupitia kijiji hicho vijana 
wataendelea na masomo hata kama wanachunga mifugo yao kutokana na 
kupatiwa tablet ambazo zitawawezesha kujifunza hata wakiwa nje 
wakichunga mifugo yao.
Aidha
 miongoni mwa manufaa makubwa yatakayopatikana katika mradi huo wa 
kijiji cha digitali ni kuweza kupata nishati rahisi na iliyo rafiki kwa 
mazingira kwa kuwepo na jenereta linalotumia nishati ya jua.Kuwepo kwa 
kijiji hicho kunataka kudhihirisha ni kwa namna gani teknolojia inaweza 
kutumika kuleta mabadiliko chanya yanayotakiwa kwa ajili ya maendeleo ya
 wananchi waliopo vijijini.
Kijiji
 hicho cha Loliondo ambacho kitakuwa cha nne katika vijiji vya 
kidigitali barani Afrika kimeelezwa naMkuu wa mkoa wa Arusha Mheshimiwa 
Mrisho Gambo kama utekelezaji wa Sera ya Tiba Mtandao kutokana na 
kuzinduliwa kwa Kliniki Mtandao iliyopo katika Kijiji hicho.Katika 
uzinduzi wa mradi huo kwa ujumla wake, kliniki ndicho kitu ambacho 
kinaonekana kwenda karibu zaidi na wananchi wa Ololosokwan kwani itakuwa
 inatoa huduma za afya, bora za kisiasa na za haraka kwa wakazi wa kata 
za Soitsambu naa Oloipiri, Wilayani Ngorongoro.
Katika
 hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa mkoa wa Arusha ,Waziri wa 
Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Mhe Ummi Mwalimu 
wakati wa uzinduzi wa kliniki hiyo,alisema kuwa Tiba Mtandao imekua ni 
miongoni mwa Vipaumbele vya Wizara yake ili wananchi wote Tanzania 
waweze kupata huduma stahiki za matibabu pasipo kujali changamoto za 
Kijiografia zinazotukabili,
Pamoja
 na kufanya uzinduzi huo katika hotuba yake Mkuu wa mkoa wa Arusha, 
Mrisho Gambo aliwashukuru wote walioshiriki kuleta Mradi huo wa maana 
kwa mkoa wa Arusha kwani wangeweza kupeleka sehemu nyingine yeyote na 
kuongeza kuwa ni deni kubwa sana lazima tuhakikishe huduma hiyo 
imefanikiwa.
Akizungumzia
 masuala ya afya kama kipaumbele katika mradi huo wenye lengo la 
kuhifadhi utamaduni wa kimasai huku wakitumia teknolojia ya kisasa 
kuleta maendeleo katika elimu na kuhifadhi mazingira, Mkuu huyo wa mkoa 
akizungumza kwa niaba ya Waziri alisema kuwa kutokana na umuhimu wa 
sekta ya afya kwa kila Mtanzania ,serikali itaelekeza nguvu katika 
Kliniki hiyo ili kuiwezesha kutoa huduma stahiki na Kwa muda mrefu kwa 
wananchi wa maeneo haya.
"Kliniki
 hii ni ya kwanza Tanzania na itaweza kutoa huduma bora na za kisasa kwa
 njia ya mtandao kwa wananchi zaidi ya elfu kumi kutoka katika maeneo 
ambayo hapo awali wananchi walikuwa wanatembea umbali mrefu zaidi ya 
Kilomita 50 kufuata huduma za afya".
"
 Hii inadhihirisha kwamba mwananchi wa Ololosokwan na maeneo ya jirani 
anaweza kuhudumiwa na daktari bingwa aliyeko Muhimbili au kokote Duniani
 kupitia Klinik hii;na mfumo wa Mtandao uliopo unaruhusu upatikanaji wa 
huduma hizi kwa kipindi chote cha mwaka mzima".
Aidha
 aliitaka Halmashauri kutenga Bajeti kwa ajili ya kuongeza hadhi ya 
zahanati hiyo kuwa Kituo cha Afya ambapo itaenda sambamba na kuongeza 
majengo Pamoja na wataalam watakaoweza kutoa huduma stahiki Kwa 
wananchi.
Upatikanaji
 wa kituo cha Afya katika eneo hilo huku kukiwepo na kliniki mtandao 
kutasaidia kuokoa maisha ya wananchi ambao wengi wao waliamini kupona 
magonjwa makubwa ni mpaka uende KCMC au Muhimbili tu.
Awali
 akizungumza katika uzinduzi huo Mkuu Shirika la Umoja wa mataifa 
linaloshigulikia Elimu na Sayansi (UNESCO) nchini Tanzania Bi. Zulmira 
Rodrigues alisema kijiji hicho ni ushuhuda tosha wa ukuaji wa teknolojia
 unaenda sambamba na maono ya shirika la Unesco la kutoa kipaumbele 
katika miradi ya sayansi inayosaidia wananchi wenye mahitaji moja kwa 
moja.
Alisema
 kwa kutambua adha waliyokuwa wanaipata wananchi wa Ololosokwan 
walitengeneza mradi ambao sehemu mojawapo ni kliniki Mtandao ili kuleta 
mabadiliko ya afya za watu kwa njia ya kisayansi.
Naye
 mkurugenzi wa Tiba Kutoka Wizara ya Afya Dr. Margareth Evelyne Mhando 
alishukuru Unesco kusaidia kutekeleza malengo ya Wizara kupitia Mradi 
huu wa kijiji cha digitali na kuongeza kuwa ni hatua nzuri katika sekta 
ya afya Kwa sababu hivi sasa wananchi waliombali na vituo vya Afya 
kupitia Mradi huu watapata huduma bora kutoka Kwa matabibu wabobezi.
Uzinduzi
 wa Mradi huu ulihudhuriwa pia na Balozi wa Switzerland Nchini Tanzania 
Bi. Florence Mattli, Wawakilishi wa Samsung ambao ndio waliotoa fedha na
 Teknolojia pamoja na wawakilishi kutoka Umoja wa Ulaya (EU).
Bi.
 Mattli alisema kwamba wataendelea kusaka wadau wengine kuhakikisha 
kwamba mradi huo unaendelea kutanuka na kufanikiwa kwa kujazia maeneo 
ambapo panahitaji nguvu nyingine.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni