
Ilikuwa
 kama mchezo wa kuigiza kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro baada 
ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, Emmanuel 
Mkumbo kufikishwa ili apandishwe kizimbani kujibu mashtaka sita, 
likiwamo la kutishia kuua. 
Tukio
 zima la kumpeleka mahakamani, kumpandisha kizimbani na kumsomea 
mashtaka kwa muda wa dakika 30 hivi lilitawaliwa na vituko. Kwanza, ni 
jaribio la kuwaficha wanahabari. 
Kabla
 ya kufikishwa mahakamani, Polisi mkoani Morogoro iliwaarifu wanahabari 
kuwa ingetoa taarifa kuhusu mkurugenzi huyo lakini saa 4:30 asubuhi 
wakati Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro,
 Ulrich Matei akijiandaa kuzungumza nao, alipigiwa simu akatoka nje ya 
ukumbi na aliporejea alisema hawezi kutoa taarifa tena na akaondoka. 
Waandishi
 walipofika mahakamani saa 5:00 asubuhi walikuta Kamanda Matei akishuka 
kwenye gari na alipanda tena akasogea kando kuzungumza na baadhi ya 
askari wake. 
Pili,
 baada ya hakimu kumaliza kusikiliza kesi hiyo, Mkumbo hakurudishwa 
mahabusu mahakamani hapo kama ilivyo ada ili kusubiri utaratibu mwingine
 badala yake mshtakiwa huyo alihamishiwa chumba cha hakimu ambacho 
hakikuwa na kesi inayoendelea. 
Humo
 ndugu zake walimpelekea koti kubwa jeusi na kofia aina ya pama, hivyo 
alitoka akiwa tofauti na alivyoingia akiwa na fulana yenye rangi nyeupe,
 bluu na nyeusi. Baada ya kuvaa alitoka akiwa amezingirwa na polisi, 
huku ndugu wakiwazuia wanahabari kumpiga picha. 
Mashtaka dhidi yake
Mkumbo
 ambaye ni mkazi wa Tegeta jijini Dar es Salaam alipandishwa kizimbani 
kujibu mashtaka sita, la kwanza likiwa la kutishia kuua kwa bastola na 
la pili ni la usalama barabarani lenye makosa matano.
Alisomewa
 mashtaka hayo na mawakili wa Serikali Sunday Hyera na Edgar Bantulaki. 
Katika shtaka la kwanza, mbele ya hakimu Agripina Kimaze anadaiwa Oktoba
 15, saa 10:30 jioni alitenda kosa la kutishia kuua eneo la Mkambarani, 
Manispaa ya Morogoro.
Anadaiwa
 katika shtaka hilo la jinai namba 226 la mwaka 2016, alitishia kumuua 
kwa bastola askari namba 5057, Koplo Tuti Ndaga wa Kikosi cha Usalama 
Barabarani Mkoa wa Morogoro, kinyume na kifungu namba 89 (1),(2),(a) cha
 Sheria ya Kanuni ya Adhabu namba 16. 
Katika shtaka la pili la ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani lenye makosa matano, ilidaiwa kuwa; kwanza, siku na muda huo eneo la Mbuyuni Mkambalani, mshtakiwa alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Prado lenye rangi ya kijivu bila kuwa na leseni.
Katika shtaka la pili la ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani lenye makosa matano, ilidaiwa kuwa; kwanza, siku na muda huo eneo la Mbuyuni Mkambalani, mshtakiwa alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Prado lenye rangi ya kijivu bila kuwa na leseni.
Pili,
 ilidaiwa alikuwa akiendesha gari hilo ambalo halikuwa na bima; tatu, 
alikutwa akiendesha kwa mwendo kasi; na nne, alikataa kupeleka gari 
Kituo cha Polisi cha Kingoluwira kama alivyoamriwa na askari, WP namba 
5392 Sajenti Anna. 
Ilidaiwa
 katika shtaka la tano kwamba, wakati akiendesha alisimamisha gari 
katikati ya barabara kuu ya Morogoro-Dar es Salaam kwa uzembe, bila 
uangalifu wala kuzingatia watumiaji wengine wa barabara. Mkurugenzi huyo
 alikana mashtaka yote yanayomkabili.
Hakimu
 Kimaze alitoa masharti ya dhamana kwa mshtakiwa kwamba awe na mdhamini 
mmoja kwa kila shtaka, yaani shtaka la jinai na la usalama barabarani 
lenye makosa matano, wote wawe wakazi wa Morogoro na mmoja akitakiwa 
kuweka dhamana ya Sh500,000 kwa kosa la kwanza na Sh1 milioni kwa kosa 
la pili. 
Mshtakiwa alikidhi masharti ya dhamana na kuachiwa huru, huku gari likiendelea kushikiliwa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Morogoro.
Mshtakiwa alikidhi masharti ya dhamana na kuachiwa huru, huku gari likiendelea kushikiliwa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi Mkoa wa Morogoro.
Hakimu
 Kimaze aliahirisha shauri hilo hadi Oktoba 31, usikilizwaji wa awali 
utakapoanza baada ya upande wa mashtaka kudai upelelezi umekamilika. 

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni