Hatimaye
 mazishi ya kuuaga mwili wa Meya wa zamani wa Jiji la Dar es Salaam, Dk.
 Didas Masaburi, yamewakutanisha Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa 
na Rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete kwa kusalimiana na 
kushikana mikono.
Tukio
 hilo la aina yake liliwafanya watu mbalimbali waliokuwa katika msiba 
huo kubaki wakishangaa, hasa baada ya Rais mstaafu Kikwete kumfuata 
Lowassa na kumwuliza hali rafiki yake huyo wa zamani waliokulia wote 
CCM.
Tangu
 wakati huo viongozi hao ambao walikuwa marafiki wa karibu tangu ujana 
wao walikuwa wakirushiana vijembe ambapo jana walikutana ana kwa ana 
katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam wakati wa kuuaga mwili 
wa Dk. Masaburi kabla ya kwenda kuzikwa nyumbani kwake Chanika Manispaa 
ya Ilala.
Akiwa
 katika viwanja hivyo, Kikwete alipomwona Lowassa akiingia viwanjani 
hapo alinyanyuka na kumfuta Lowassa katika kiti chake kisha kusalimiana 
naye kwa kupeana mikoni huku wakizungumza.
Lowassa
 aliyekuwa ameketi jirani na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana 
pamoja na mkewe Regina Lowassa, alisimama na kumjibu salamu.
Kwa
 muda mrefu wanasiasa hao ambao wamewahi kuwa marafiki hadi kupewa jina 
la utani ‘Boys II Men’, waliingia katika uhasama kwa kile kinachodaiwa 
ni kusalitiana kisiasa.
Urafiki
 wa wawili hao ulianza kuingia doa mwaka 2008 wakati wa kashfa ya 
Richmond iliyosababisha Lowassa kujiuzulu uwaziri mkuu kwa kile 
alichoeleza ni kunyimwa haki ya kusikilizwa baada ya kuibuka kwa kashfa 
hiyo kwa kile alichodai ilikuwa ni vita ya kutaka ‘uwaziri mkuu’.
Ukaribu
 wa Lowassa na Kikwete uliendelea kupungua na kuwa shakani zaidi wakati 
wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana baada ya Lowassa kukatwa jina lake katika
 kinyang’ anyiro cha kuwania nafasi ya kugombea urais kupitia Chama Cha 
Mapinduzi (CCM) na kuamua kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo 
(Chadema).
Kwa
 takribani mwaka mmoja sasa tangu mchakato wa ndani wa CCM wa kumpata 
mgombea wake wa urais Julai 10, mwaka jana umalizike wawili hao 
hawajawahi kukutana hadharani na kupeana mikono.
Katika
 mchakato huo Kamati Kuu ya CCM iliyokutana hadi usiku wa manane 
iliibuka na jibu kwamba, jina la Edward Lowassa limekatwa katika watu 
wanaowania urais kupitia chama hicho.
Waliopitishwa
 na kuingia tano bora na Kamati Kuu walikuwa ni Bernard Membe, Dk John 
Magufuli, Dk Asha Rose Migiro, January Makamba na Amina Salum Ali, huku 
makada wengine 33 wakitupwa akiwamo Lowassa.
Kutokana
 na hali hiyo Lowassa alichukua aumuzi mzito wa kuihama CCM, Julai 28, 
mwaka jana na kujiunga na Chadema na hatimaye kuteuliwa kuwa mgombea 
urais kupitia chama hicho cha upinzani akiungwa mkoano na vyama vinaunda
 Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni