Waziri
 wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (wa nne kutoka kushoto) akiwa 
katika picha ya pamoja na Mawaziri wenzake wa Fedha kutoka nchi 54 za 
Kiafrika, wanaohudhuria Mkutano wa 5 wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya 
Korea na nchi za Afrika (KOAFEC), unaofanyika Jijini Seoul, Korea 
Kusini.
Waziri
 wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (kushoto) na Mkurugenzi 
Mtendaji wa Benki ya Maendeleo Afrika anayeiwakilisha Tanzania (AfDB) 
Dkt. Nyamajeje Weggoro (katikati) wakimsikiliza kwa makini Raisi wa 
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kabla ya kuanza kwa mkutano 
unaojadili namna kilimo na mapinduzi ya viwanda vinavyoweza kuibadili 
Afrika Kiuchumi na Kijamii wakati wa Mkutano wa 5 wa Ushirikiano wa 
Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika (KOAFEC) unaofanyika Jijini 
Seoul, Korea Kusini.
Waziri
 wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (kulia) akitia saini 
makubaliano ya uteuzi wa mradi utakao fadhiliwa kwa pamoja kati ya Benki
 ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Serikali ya Korea, wenye thamani ya 
dola Milioni 50 za Marekani sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 100.18 
zitakazotumika kujenga njia ya usafirishaji umeme kwanjia ya gridi ya 
Taifa, yenye msongo wa kV 400 katika ukanda wa kaskazini Magharibi 
itakayoanzia mkoani Mbeya, Nyakanazi hadi Mkoani Kigoma.
 
 
Waziri
 wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango  (Mb) (katikati) akiwa na 
Mawaziri wenzake kutoka nchi za Kenya, Uganda na Ethiopia (wengine 
hawako Pichani) wakionesha kwa waandishi wa habari (hawako pichani pia) 
nyaraka za makubaliano ya uteuzi wa mradi utakao fadhiliwa kwa pamoja 
kati ya Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Serikali ya Korea, wenye 
thamani ya dola Milioni 50 za Marekani sawa na zaidi ya shilingi Bilioni
 100.18 zitakazotumika kujenga njia ya usafirishaji umeme kwa njia ya 
gridi ya Taifa, yenye msongo wa kV 400 katika ukanda wa kaskazini 
Magharibi kwa upande wa Tanzania itakayoanzia mkoani Mbeya, Nyakanazi 
hadi Mkoani Kigoma. wakati wa Mkutano wa 5 wa ushirikiano wa Kiuchumi 
kati ya Korea Kusini na nchi za Kiafrika, unaoendelea Jijini Seoul Korea
 Kusini.
 
 
Waziri
 wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kushoto, na 
Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini, Lee 
Duk-Hoon, wakitia saini  Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola 
za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194 za 
Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa maji 
taka Jijini Dar es salaam, wakati wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi 
kati ya Korea na nchi za Afrika, unaoendelea Jijini Seoul, Korea Kusini
 
 
Waziri
 wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kushoto, na 
Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini, Lee 
Duk-Hoon, wakipeana mikono baada ya kusaini  Mkataba wa mkopo wenye 
masharti nafuu wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya 
shilingi Bilioni 194 za Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa 
Miundombinu ya mfumo wa maji taka Jijini Dar es salaam, wakati wa 
Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika, 
unaoendelea Jijini Seoul, Korea Kusini
 
 
Waziri
 wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), kushoto, na 
Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki ya EXIM ya Korea Kusini, Lee 
Duk-Hoon, wakionesha mkataba waliousaini wa mkopo wenye masharti nafuu 
wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194
 za Tanzania, kwa ajili ya mradi wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa 
maji taka Jijini Dar es salaam, wakati wa Mkutano wa Ushirikiano wa 
Kiuchumi kati ya Korea na nchi za Afrika, unaoendelea Jijini Seoul, 
Korea Kusini
 
 
Baadhi
 ya wajumbe kutoka Tanzania na Korea walioshuhudia utiawaji saini wa 
mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za marekani milioni 90.092
 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 194 za Tanzania, kwa ajili ya mradi 
wa Upanuzi wa Miundombinu ya mfumo wa maji taka Jijini Dar es salaam, 
wakati wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea na nchi za 
Afrika (KOAFEC), unaoendelea Jijini Seoul, Korea Kusini.
                                                                    Benny Mwaipaja, WFM, Seoul, Korea 
TANZANIA,
 Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Korea ya Kusini zimetiliana 
saini makubaliano ya pamoja kutekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya umeme 
gridi ya Kaskazini Magharibi inayoanzia mkoani Mbeya, Nyakanazi hadi 
Kigoma, yenye msongo wa kV 400 mbapo Serikali ya Korea imeahidi kutoa 
Dola zaMarekani milioni 50 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 100.18, kwa
 ajili ya kugharamia mradi huo. 
Hali kadhalika, Tanzania na 
Benki ya Exim ya Korea, zimesaini  Mkataba wa mkopo wenye masharti nafuu
 wa Dola za marekani milioni 90.092 sawa na zaidi ya shilingi Bilioni 
194 za Tanzania, kwaajili ya mradi wa Upanuzi waMiundombinu ya mfumo wa 
maji taka Jijini Dar es salaam. 
Kwa upande wa Tanzania, 
Makubaliano pamoja na Mkataba vimesainiwa na Mhe. Dkt. Philip Mpango 
(MB) Waziri wa Fedha na Mipango kwa niaba ya Serikali, Oktoba 25, 2016 
Jijini Seoul nchini Korea Kusini huku upande wa AfDB, aliye saini ni 
Rais wa Benki hiyo Adesina Akinwumi, na kwa upande wa Benki ya Exim, 
mkataba huo umesainiwa na Mwenyekiti ambaye pia ni Rais wa Benki hiyo 
Lee Duk-Hoon. 
Akizungumza mara baada ya kutia saini makubaliano 
na mkataba huo, Dkt. Mpango amesema makubaliano na mkataba 
vilivyosainiwa vina manufaa makubwa kwa wananchi wa Tanzania. 
“Wananchi
 wa Upande ule waanze kufurahia kwamba maendeleo yanakuja na hasa 
tunaposema maendeleo ya viwanda ambavyo nilazima vitumie umeme, na 
kwamba mradi huu unatarajia kupelekwa hadi Mbeya” Amesisitiza Dkt. 
Mpango. 
Dkt. Mpango, amesema kuwa mradi huo una umuhimu mkubwa 
pia kwakuwa serikali imedhamiria kuufungua ukanda wa Magharibi mwa 
Tanzania, kwa upande wa viwanda vya aina mbalimbali. 
Kwa upande 
wake, Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Uwekezaji) wa Shirika la Ugavi wa Umeme
 nchini Tanzania-TANESCO, Decklan Mhaiki, amesema mradi wa umeme wa 
Nyakanazi hadi Kigoma utakuwa na urefu wa kilometa 280 na utakapo 
kamilika utaondoa changamoto ya shirika hilo kuzalisha umeme unatumika 
katika ukanda huo wa Magharibi hususan Kigoma, kwa kutumia majenereta 
ambayo uendeshaji wake ni ghali na umeme wake si wa uhakika. 
“Kuleta
 laini kama hii, kwanza itapunguza gharama kubwa, na umeme wa ziada 
utakao zalishwa tunaweza kuuza nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia 
Congo, upande wa pili wa Ziwa Tanganyika, lakini kikubwa ni 
kuwahakikishia wananchi wa mkoa wa Kigoma kuwa na umeme wa uhakika” 
ameongeza Bw. Mhaiki. 
Akizungumzia mkataba wa ujenzi wa 
miundombinu ya maji taka Jijini Dar es salaam, Dkt. Philip Mpango, 
amebainisha kuwa mradi huo unatarajia kuwa na tija kwakuwa utatatua 
changamoto ya majitaka kutuama mitaani hasa wakati wa mvua na 
kusababisha magonjwa ya mlipuko kikiwemo kipindupindu. 
Akifafanua
 kuhusu mradi huo, Mchumi ambaye pia ni  Afisa anayeshughulika na 
utafutaji wa Fedha za Nje kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Melckzedek 
Mbise, amesema kuwa mradi wa maji wa Ruvu  unatarajia kuongeza wingi wa 
maji Jijini Dar es salaam, utakaosababisha uzalishaji wa maji taka pia 
kuongezeka, hivyo mradi huo wa kuondoa maji taka umekuja wakati muafaka.
 
“Mradi huu umekuja wakati muhimu na mkopo una masharti nafuu sana” Amesisitiza Bw. Mbise. 
Naye
 Afisa Mkuu wa utafutaji rasilimali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango 
Zanzibar, Sabra Issa Machano, amesema kuwa  kati ya nchi 54 za Kiafrika 
zinazohudhuria mkutano wa Tano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Korea 
naAfrika, Mjini Seoul Korea, ni nchi nne tu zilizopewa mkopo na ufadhili
 ambazo ni Kenya, Uganda na Ethiopia, huku Tanzania ikipewa kiasi 
kikubwa zaidi cha fedha jambo linaloonesha kuwa Tanzania inakubalika 
Kimataifa. 
 
 
 
 
  
 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni