ASOTEA MAFAO YAKE MIAKA NENDA RUDI


Mfanyakazi mmoja wa  ofisi ya Kituo cha Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo,kanda ya kaskazini,kilichopo jijini Arusha, Kandidi Mlingi,ambae alipata ajali ya gari mwaka 2015 na kukatwa mkono wake wa kushoto hadi leo anasotea malipo ya fidia ya ajali hiyo. 

Mlingi, ambae Septemba 18 mwaka 2015,majira ya saa 11.30 jioni ,wakati wa ajali alikuwa akitokea eneo la Lokii wilayani Arumeru kukagua minada ya mifugo akiwa na watumishi wenzake walikuwa wakisafiria kutumia gari aina ya Toyota Land Cruiser, namba STJ 5929.
 
Gari hiyo ilikuwa ikiendeshwa na Samweli Kambaine,iliacha njia na kupinduka kwenye bara bara itokayo Lokii wilayani Arumeru ikirejea kwenye kituo cha utafiti wa magonjwa ya mifugo kanda ya kaskazini mjini Arusha . 

Miongoni mwa wafanyakazi wengine waliopata ajali kwenye msafara huo ni pamoja na  Nemes Msaki,ambapo yeye  alipata majeraha kwa asilimia 17 huku Kandidi alipata majeraha kwa asilimia 54 na dereva alipoteza fahamu.
 
Kulingana na uchunguzi uliofanywa na daktari wa Hospital ya mkoa ya Mount Meru, Dkt Iddi Mtengwa ,umebaini kiwango hicho cha majeraha waliyopata wafanyakazi hao sanjari na aliyekuwa dereva kupoteza fahamu.
Ripoti ya askari wa kikosi cha usalama barabarani cha wilaya ya Arumeru, kilichopo mji mdogo wa Usa river,walithibitisha kuwa ajali hiyo ilikuwa ni mbaya na gari hilo halifai tena .
 
Taarifa toka ndani ya familia zimeeleza kusikitishwa kwao na wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi,kutokuwa na mawasiliano na mtumishi huyo ambae kwa sasa hana mkono mmoja .
 
Mke  wa majeruhi Kandidi amesema tangu kutokea ajali hiyo Septemba 2015 hakuna jitihada zozote zinazofanywa na Wizara husika  juu ya namna ya kumwekea mkono bandia mume wake wala mawasiliano .
 
 
 
ARUSHA
WALIOKUWA wafanyakazi wa kiwanda cha nguo cha Kilitex cha jijini Arusha,wamemuomba rais John Magufuli, awasaidie waweze kulipwa stahiki zao ambazo hawakulipwa hadi leo tangia kiwanda hicho kisitishe uzalishaji na kufungwa rasmi mwaka 2007.
 
Wakizungumza na wanahabari, jijini Arusha,Mwenyekiti wa wa Wafanyakazi hao Shabaan Tandala, na katibu wake Nathaniel Longida, wamesema wameshapeleka kilio chao hicho kwa mamlaka mbalimbali za serikali lakini hadi leo hawajapata ufumbuzi .
 
Wamesema katika harakati zao hizo walijibiwa na Ikulu kwa barua kumb namb  STJ/MIL/1 ya 29/2/2007ambapo Ikulu iliandikia Wizara ya Fedha kwa barua namb  CEA/404/10/01 ya 8/10/2007iliyosainiwa na aliyekuwa katibu wa rais, Masaju,kwenda wizara ya fedha ili waweze kulipwa lakini hadi leo .
 
Wamesema Novemba 26/2007 walipokea barua nyingine toka Ikulu namb C/CA 251/473/01 iliyosainiwa na Mahushi kwa niaba ya Katibu mkuu Hazina  ikisisitiza   kulipwa stahiki zao ,ambazo hawajalipwa  hivyo wamelazimika kupeleka kilio chao kwa rais Magufuli,ili awasaidie wapate stahiki hizo.
 
Kwenye barua yao ya wamemuomba rais kuwasaidia kupata stahiki hizo kwa kuwa kuna dalili za kutopata stahiki zao.
 
Wamesema mwezi May mwaka 2015 ,walimkabidhi barua yao Katibu mkuu wa CCM, Abdulhaman Kinana ,wakimuomba awasaidie kuifikisha kilio chao kwa rais Jakaya Kikwete, ili waweze kulipwa lakini hadi leo kimya.
 
Wamesema kutokana na ukimya huo ambao unawajengea hofu na mashaka kutokana na kutolipwa wanamuomba rais Magufuli, awasaidie waweze kupata stahiki zao.
 
Wamesema wakati kiwanda kinabinafisishwa kupitia PCRC, walikuwa waanyakazi zaidi ya 200 lakini sasa wamebakia wachache kwa kuwa wengine wamefariki dunia bila ya kulipwa stahiki zao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni