Mahakama
 ya hakimu mkazi  Arusha, imeiagiza serikali kukamilisha upelelezi wa 
kesi ya uchochezi inayomkabili mbunge wa jimbo la Arusha, Godbless Lema,
 Chadema, ndani ya siku 60 ambapo imepangwa Novemba 15 mwaka huu 
vinginevyo itatoa maamuzi mengine.
Hakim
 mkazi mfawidhi, Augostino Rwezile, ametoa agizo hilo leo katika 
mahakama hiyo ambayo ilikuwa imekaa tayari kwa kuanza kusikiliza kesi 
hiyo kabla ya wakili wa serikali kuomba iahirishwe kutokana na upelelezi
 kutokukamilika.
Awali
 wakili wa serikali Blandina Msawa, aliiambia mahakama hiyo kuwa 
upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba  kupewa siku 60 ili 
kukamilisha upelelezi huo.
Wakili
 wa mlalamikajhi, John Malya, ameiambia mahakama kuwa anashangaa kuona 
upelelezi unachukua muda mrefu wakati simu ya mbunge huyo imeshikiliwa 
na polisi kwa kipindi kirefu.
Ameiambia
 mahakama kuwa simu hiyo ndio iliyotumika kusambaza maneno ya uchochezi 
kama inavyodaiwa na serikali, hivyo yeye anashangaa kuona kesi ikichukua
 muda mrefu 
Kwa
 upande wake Lema, ameiomba mahakama kumpatia muda wa kutosha ili aweze 
kuhudhuria vikao vya bunge la Jamhuri mwezi ujao mjini Dodoma, ili aweze
 kupata muda pia wa kuhudhuria kesi yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni