MAHAKAMA IMEAGIZA SERIKALI KUKAMILISHA UPELELEZI WA KESI YA MBUNGE LEMA


Image result for picha za mbunge lema

Mahakama ya hakimu mkazi  Arusha, imeiagiza serikali kukamilisha upelelezi wa kesi ya uchochezi inayomkabili mbunge wa jimbo la Arusha, Godbless Lema, Chadema, ndani ya siku 60 ambapo imepangwa Novemba 15 mwaka huu vinginevyo itatoa maamuzi mengine.

Hakim mkazi mfawidhi, Augostino Rwezile, ametoa agizo hilo leo katika mahakama hiyo ambayo ilikuwa imekaa tayari kwa kuanza kusikiliza kesi hiyo kabla ya wakili wa serikali kuomba iahirishwe kutokana na upelelezi kutokukamilika.

Awali wakili wa serikali Blandina Msawa, aliiambia mahakama hiyo kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba  kupewa siku 60 ili kukamilisha upelelezi huo.

Wakili wa mlalamikajhi, John Malya, ameiambia mahakama kuwa anashangaa kuona upelelezi unachukua muda mrefu wakati simu ya mbunge huyo imeshikiliwa na polisi kwa kipindi kirefu.

Ameiambia mahakama kuwa simu hiyo ndio iliyotumika kusambaza maneno ya uchochezi kama inavyodaiwa na serikali, hivyo yeye anashangaa kuona kesi ikichukua muda mrefu

Kwa upande wake Lema, ameiomba mahakama kumpatia muda wa kutosha ili aweze kuhudhuria vikao vya bunge la Jamhuri mwezi ujao mjini Dodoma, ili aweze kupata muda pia wa kuhudhuria kesi yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni