Wakazi wa Kijiji cha Kisesa Kata ya Vudee wakishuhudia zoezi la uteketezaji wa shambala Mirungi
Mkulima
 wa zao la Mirungi Johnson Charles Kangara akiwa ameshika mafuta ya taa 
tayari kwa ajili ya kuteketeza shamba lake la Mirungi
 Shamba la Mirungi likiteketea baada ya agizo la Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe Rosemary Staki
 Dc Staki akiwasisitiza wananchi kutojihusisha na kilimo cha zao la Mirungi
Na Mathias Canal, Kilimanjaro
Mwishoni
 mwa mwezi Septemba mwaka huu Uongozi wa Wilaya ya Same ulitangaza vita 
dhidi ya wakulima wa Bangi, na Mirungi huku akitangaza kuwa kifungo cha 
miaka 30 kitawahusu wakulima wote wanaojishughulisha na kilimo hicho 
haramu kwani Bangi na Mirungi ni hatari kwa afya za watumiaji na 
kuisababishia serikali hasara kwa kutopokea Kodi.
Kiama
 hicho kilitangazwa na Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe Rosemary Staki 
Senyamule wakati akikabidhiwa mradi wa Ruvu muungano uliojumuisha 
zahanati sita, Nyumba mbili za waganga, matanki saba ya kuvuna maji na 
madarasa 54, ofisi 16 za walimu, vyumba na vyoo vya chuo cha ufundi 
makanya uliofadhiliwa na shirika la World Vision Tanzania.
Dc
 Staki alisema kuwa kwa asilimia kubwa serikali imekuwa ikiwadhibu 
wanaoingiza Mirungi na Bangi sokoni huku ikiwasahau kuwachukulia hatua 
wale wote wanalima zao hilo.
Hivi
 karibu katika kijiji cha kisesa kata ya Vudee Wilayani humo ilibainika 
kuwa kuna wakulima wa Mirungi ambao wanajihusisha na zao hilo kwa muda 
mrefu pasina serikali kuwabaini na kuwa sugu kwa kilimo hicho hatimaye 
kukiona kama kilimo cha halali.
Dc Staki alipotangaza kiama cha kukabiliana na wale wote wanaojihusisha na kilimo hicho aliahidi kuwatafuta wakulima hao na hatimaye kuwachukulia hatua za kisheria na kuhakikisha kuwa Wilaya ya same inakuwa safi pasina kuwa na Mirungi.
Hata hivyo katika ziara yake ya kazi Mhe Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki alipozuru kijiji cha kisesa kata ya Vudee alifanikiwa kumuweka chini ya ulinzi mkulima wa zao la Mirungi Johnson Charles Kangara na hatimaye kumuelekeza kuwasha kiberiti yeye mwenyewe katika shamba zima na kuchoma zao hilo.
Dc Staki ameahidi kuhakikisha Wilaya ya Same inasifika kwa kilimo cha mazao mengine rafiki katika jamii ya Biashara na chakula na kuteketeza mazao yote haramu.
Dc Staki alipotangaza kiama cha kukabiliana na wale wote wanaojihusisha na kilimo hicho aliahidi kuwatafuta wakulima hao na hatimaye kuwachukulia hatua za kisheria na kuhakikisha kuwa Wilaya ya same inakuwa safi pasina kuwa na Mirungi.
Hata hivyo katika ziara yake ya kazi Mhe Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki alipozuru kijiji cha kisesa kata ya Vudee alifanikiwa kumuweka chini ya ulinzi mkulima wa zao la Mirungi Johnson Charles Kangara na hatimaye kumuelekeza kuwasha kiberiti yeye mwenyewe katika shamba zima na kuchoma zao hilo.
Dc Staki ameahidi kuhakikisha Wilaya ya Same inasifika kwa kilimo cha mazao mengine rafiki katika jamii ya Biashara na chakula na kuteketeza mazao yote haramu.


 


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni