Kiongozi
 mkuu wa kanisa la Ukombozi ,Nabii B.G Malisa   akizungumza na waandishi
 wa habari mara baada tu ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa
 wa Kilimanjaro(KIA) leo ambapo atakuwa na mkutano wa maombezi wa siku 8
 katika viwanja vya reli jijini Arusha
 Umati wa wakazi wa 
mkoa
 wa Arusha waliofurika katika uwanja wa ndege wa kimatifa wa 
Kilimanjaro(KIA) kumpokea Nabii B.G Malisa ambaye atakuwa na mkutano wa 
maombezi wa siku 8 katika viwanja vya reli jijini A
rusha
Na Mahmoud Ahmad,Arusha
 Watanzania
 wametakiwa kudumisha amani ya nchi kwa kuepuka kufanya matukio ambayo 
yanaweza kuchochea vurugu na hatari ya kuliingiza taifa katika hali ya 
machafuko. 
Wito
 huo umetolewa jana na mchungaji kiongozi wa kanisa la Ukombozi hapa 
nchini, Nabii B. G Malisa wakati alipokuwa akihubiri neno la Mungu 
katika viwanja vya reli jijini Arusha. 
Nabii Malisa alisema kwamba watanzania wana jukumu kubwa la kuhakikisha wanaombea amani ya nchi inaendelea kutawala hapa nchini.
Alisema
 ya kwamba amekuwa akifanya ziara mbalimbali katika nchi mbalimbali 
duniani na kushuhudia hali ya usalama ikiwa tete ambapo askari wamekuwa 
wakitembea mitaani huku wameshika silaha za moto. 
"Hivi
 karibuni nilikuwa Nigeria wakati nashuka uwanja wa ndege nilipokelewa 
na askari wenye silaha za moto nikajiuliza maswali mengi sana kuhusu 
amani tuliyonayo hapa Tanzania "alisema Malisa 
Hatahivyo,
 alitoa wito kwa serikali kuunga mkono juhudi za viongozi mbalimbali wa 
dini hapa nchini katika kuwasaidia vijana na kusema viongozi wa dini 
wanafanya kazi kubwa katika kuwainua watu kiuchumi na kuwaepusha na 
vitendo viovu. 
Awali
 akizungumza na waandishi wa habari mchungaji wa kanisa la Ukombozi tawi
 la Arusha Mchungaji Ushindi alisema kwamba mhubiri huyo atakwenda 
kufanya huduma ya maombezi mkoani Arusha kwa siku nane na kuwataka 
wakazi hao kujitokeza kwa wingi
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni