TPRI:WADAU WOTE WA KILIMO TUMIENI VIWATILIFU VILIVYOSAJILIWA.

Habibu Mkalanga ,katika ofisi ya msajili viwatilifu (TPRI)na mratibu wa mafunzo mkoani Arusha.
                                                   Na Mahmoud Ahmad Arusha.
Wito umetolewa kwa wadau wote wa kilimo watumie viwatilifu vilivyosajiliwa na Taasisi ya viwatilifu ya kufanya utafiti katika nchi za kitropiki (TPRI)kwani ubora wake umehakikiwa na jinsi vinavyofanya kazi umehakikiwa pia.
Kauli hiyo imetolewa na Habibu Mkalanga katika ofisi ya msajili wa viwatilifu na mratibu wa mafunzo mkoani Arusha na kusema kuwa kabla ya kutumia viwatilifu ni muhimu watumiaji waangalie matumizi kwenye vibandikao kama viwatilifu hivyo ni vya wadudu au magugu,aina mavazi wanayotakiwa kuvaa kabla ya kunyunyiza viwatilifu,kiasi kinachotakiwa, kisiwe chini ya kiwango wala juu ya kiwango.
Habibu amesema ni vyema mkulima akachukua tahadhari mapema, afahamu  siku ngapi anaweza kuvuna mazao yake baada ya kunyunyiza viwatilifu ili asiweze kupata madahara baada ya kuvuna vinavyosababishwa na masalia ya viwatilifu katika mazao 
Amesema kuwa TPRI ipo ili kuthibitisha viwatilifu vinafanya kazi kama inavyokusudiwa , ili kuhakikisha havileti madahara kwa binadamu,wanyama,na mimea ,sambamba na kutokuvunja sheria ya uthibiti wa visumbufu vya mimea ya mwaka 1997 ambapo sheria hii imeainisha makosa na adhabu ikiwemo kifungo na faini.
"Kwa mfano kuuza kiwatilifu ambacho hakina kibandiko cha maandishi ya kiswahili na kiingereza ni kinyume cha sheria kipengele chake cha 20 ya sheria ya usumbufu wa mimea faini yake ni shilingi za Kitanzania 2,000,000 "alisisitiza Habibu.
"Unajua viwatilifu ni sumu ingawaje vinafaida kubwa,ndiyo maana tunasema tahadhari kubwa ichukuliwe  na vitumiwe kama sheria inavyovitaka,lakini mtu akikaidi na kufanya atakavyo yeye sheria itachukua mkondo wake".alisema Habibu.
Aidha amesema kuwa (TPRI) imekuwa ikitoa elimu kwa njia mbalimbali kwa kutoa mafunzo kwa wadau,kwa kutoa huduma ya wima yaani kuwafuata wadau walipo,kupitia ukaguzi wa viwatilifu kwa wauzaji na kwenye maonyesho mbalimbali.

Amewataka wadau wote wa kilimo kutambua viwatilifu vilivyosajiliwa kwa kusoma maelezo yaliyoandikwa kwa lugha ya kiswahili na kiingereza kwenye vibandiko,na amewataka watambue kuwa wananchi wanalima mazao na jamii inakula mazao .pia serikali inauza mazao nje ya nchi hivyo ni vyema viwatilifu vikatumika vyema kama sheria inavyovitaka.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni