![]()  | 
| Habibu Mkalanga ,katika ofisi ya msajili viwatilifu (TPRI)na mratibu wa mafunzo mkoani Arusha. | 
                                                  
Na Mahmoud Ahmad Arusha.
Wito umetolewa kwa wadau 
wote wa kilimo watumie viwatilifu vilivyosajiliwa na Taasisi ya 
viwatilifu ya kufanya utafiti katika nchi za kitropiki (TPRI)kwani ubora
 wake umehakikiwa na jinsi vinavyofanya kazi umehakikiwa pia.
Kauli hiyo imetolewa na 
Habibu Mkalanga katika ofisi ya msajili wa viwatilifu na mratibu wa 
mafunzo mkoani Arusha na kusema kuwa kabla ya kutumia viwatilifu ni 
muhimu watumiaji waangalie matumizi kwenye vibandikao kama viwatilifu 
hivyo ni vya wadudu au magugu,aina mavazi wanayotakiwa kuvaa kabla ya 
kunyunyiza viwatilifu,kiasi kinachotakiwa, kisiwe chini ya kiwango wala 
juu ya kiwango.
Habibu amesema ni vyema 
mkulima akachukua tahadhari mapema, afahamu  siku ngapi anaweza kuvuna 
mazao yake baada ya kunyunyiza viwatilifu ili asiweze kupata madahara 
baada ya kuvuna vinavyosababishwa na masalia ya viwatilifu katika mazao 
Amesema kuwa TPRI ipo ili
 kuthibitisha viwatilifu vinafanya kazi kama inavyokusudiwa , ili 
kuhakikisha havileti madahara kwa binadamu,wanyama,na mimea ,sambamba na
 kutokuvunja sheria ya uthibiti wa visumbufu vya mimea ya mwaka 1997 
ambapo sheria hii imeainisha makosa na adhabu ikiwemo kifungo na faini.
"Kwa mfano kuuza 
kiwatilifu ambacho hakina kibandiko cha maandishi ya kiswahili na 
kiingereza ni kinyume cha sheria kipengele chake cha 20 ya sheria ya 
usumbufu wa mimea faini yake ni shilingi za Kitanzania 2,000,000 
"alisisitiza Habibu.
"Unajua viwatilifu ni 
sumu ingawaje vinafaida kubwa,ndiyo maana tunasema tahadhari kubwa 
ichukuliwe  na vitumiwe kama sheria inavyovitaka,lakini mtu akikaidi na 
kufanya atakavyo yeye sheria itachukua mkondo wake".alisema Habibu.
Aidha amesema kuwa (TPRI)
 imekuwa ikitoa elimu kwa njia mbalimbali kwa kutoa mafunzo kwa 
wadau,kwa kutoa huduma ya wima yaani kuwafuata wadau walipo,kupitia 
ukaguzi wa viwatilifu kwa wauzaji na kwenye maonyesho mbalimbali.
Amewataka wadau wote wa 
kilimo kutambua viwatilifu vilivyosajiliwa kwa kusoma maelezo 
yaliyoandikwa kwa lugha ya kiswahili na kiingereza kwenye vibandiko,na 
amewataka watambue kuwa wananchi wanalima mazao na jamii inakula mazao 
.pia serikali inauza mazao nje ya nchi hivyo ni vyema viwatilifu 
vikatumika vyema kama sheria inavyovitaka.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni