| Warembo 30 wanaoshiriki kinyanganyiro cha kumsala Miss Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara tu baada ya kutembelea ofisi za gazeti la Guardian zilizopo ndani ya mkoa wa Arusha | 
 picha ikionyesha baadhi ya warembo akiwemo mwenyeji wao ambaye ni miss Arusha wa pili kulia Maurine Ayubu wakiwa  ndani ya ofisi za gazeti la Gurdian na Nipashe zilizopo jiji Arusha
 
 Msimamizi wa kituo cha Gazeti la  Gurdian  na Nipashe mkoa wa Arusha na
 Manyara  Edward Qorro akiwa anatoa maelekezo mafupi kwa warembo juu ya 
kazi zinazofanya na magazeti hayo katika mkoa huu
 warembo ndani ya ofisi 
 Msimamizi
 wa kituo cha Gazeti la  Gurdian  na Nipashe mkoa wa Arusha na Manyara  
Edward Qorro akipokea mkoa wa Shukrani kutoka kwa Mshiriki wa mashindano
 ya miss Tanzania kutoka mkoa wa Arusha Maurine
 Ayubu ambaye pia ndio mshindi wa Miss kanda ya kaskazini mara baada 
yakumaliza kutmbelea ofisi za magazeti hayo zilizopo apa Arusha
 mkuu wa kituo siaakaamua kutumia mda huo kuji selfie na warembo 
 Meneja masoko wa gazeti la Gurdiaan   Swalehe Walii akiwa anatoa zawadi ya soda kwa mrembo Maurine Ayubu ambaye ni mwenyeji wa warembo wenzake wanaoshiriki shindano hilo kwani ametokea mkoa wa Arusha 
 warembo wakiwa wanatoka katika ofisi za gazeti la  The gurdian mara baada ya kumaliza kutembelea 
 nilipata
 wasaa wa kupiga picha na baadhi ya wakuu wa msafara wa warembo hao wa 
kwanza kabisa ni kulia mimi mwenyewe mmiliki wa blog ya libenele la 
kaskazini woinde shizza akifuatia akifuatiwa Mshiriki wa mashindano ya miss Tanzania kutoka mkoa wa Arusha Maurine
 Ayubu ambaye pia ndio mshindi wa Miss kanda ya kaskazini,wa pili 
kushoto ni muuandaaji wa  shindano la mss kanda ya mashariki Alex 
NIkitas
warembo wakitoka ndani ya ofisi za The Gardian na nipashe zilizopo mkoani Arusha
 Habari picha na Woinde Shizza,Arusha
Jumla ya 
warembo 30  kutoka mikoa mbalimbali  hapa nchi ni wanashiriki shindano 
la kumsaka mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania) leo wameingia Rasmi mkoani
 Arusha na kutembelea ofisi za gazeti la The Guardian na Nipashe  ikiwa 
ni moja ya kazi ambazo watazifanya wakiwa mkoani hapa.
Akizumza na waandishi wa habari  Mkuu wa Itifaki wa
 Miss Tanzania Albert Makoye alisema kuwa wameingia jijini hapa leo na 
wanakaa kwa muda wa siku tatu ,na katika siku hizo wanampango wa kufanya
 shughuli mbalimbali za kijamii
Aidha alisema 
kuwa pia ndani ya siku hizo tatu kutakuwa nashindano la Top model ambalo
 litafanyika Jumamosi October 15 katika ukumbi wa Triple A ulipo ndani 
ya jiji la Arusha 
"tunafanya 
shindano hilo katika ukumbi wa triple A natunarajia wananchi wengi wa 
Arusha watajitokeza kuwaona warembo hawa na kiingilio cha shindano hilo 
ni shilingi 10000 tu hivyo napenda kutumia mda huu kuwaalika wananchi wa
 Arusha kuja kumuangalia nani atakuwa Top Model"alisema Makoye 
Alisema kuwa  
mbali na hapa warembo hao wameshatembelea mikoa mbalimbali ikiwemo Mkoa 
wa Dodoma,Singinda ,Dar  es Salaam  hapa Arusha na hatimaye wanatarajia 
kuondoka na kwenda mwanza ambapo ndipo shindano hili linafayanyika kwa 
mwaka huu .
Alisema kuwa 
shindano la Miss Tanzania linatarajiwa kufanyika october 29 katika 
ukumbi wa Rock City Mall  ambapo alibainisha adi sasa warembo wote 30 
wapo vizuri na wanasubiria siku yenye ifike na maandalizi yashindano 
yamekamila
Kwa upande wake mkuu wa kituoa cha The Gardian /Nipashe mkoa wa Arusha na Manyara Edward
 Qorro alitoa shukrani kwa warembo hao kuwatambelea na kuwatakia kila la
 kheri katika mashandano hayo wanayotarajia kushiriki hivi karibuni
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni