
Wanawake wanne na wanaume tisa wamefikishwa mahakamani mjini Dodoma na kusomewa mashtaka ya mauaji ya watafiti wa Chuo cha Utafiti wa Udongo na Maendeleo ya Ardhi kilichopo Selian mkoani Arusha.
Mbele
 ya Hakimu Mkazi, Joseph Fovo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote 
kwa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma haina mamlaka kisheria 
kusikiliza kesi hiyo isipokuwa Mahakama Kuu. 
Wanadaiwa
 kuwaua Nicas Mag- azine, Theresia Nguma na Faraji Mafuru, Oktoba Mosi 
kwenye Kijiji cha Iringa Mvumi wilayani Chamwino. 
Wakili
 wa Serikali, Beatrice Nsana aliwasomea mashtaka hayo jana akidai 
walitenda kosa hilo la jinai kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha 
Sheria ya Kanuni ya Adhabu na marekebisho yake ya mwaka 2002. 
Washtakiwa
 hao ni Cecilia Mwalu, Dorca Mbehu, Edna Nuno, Grace Masaulwa, Juma 
Madeha, Albert Chimanga, Sosteness Mseche, Julius Chimanga, David 
Chimanga, Lazaro Kwanga, Yoramu Samamba, Edward Lungwa na Simon Samamba,
 wote wakazi wa Kijiji cha Iringa Mvumi.
Kesi hiyo namba 36/2016 iliahirishwa hadi Oktoba 31. Nsana alidai upelelezi haujakamilika.
Kesi hiyo namba 36/2016 iliahirishwa hadi Oktoba 31. Nsana alidai upelelezi haujakamilika.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni