NYOTA WA POP GEORGE MICHAEL AFARIKI DUNIA



Mwanamuziki nyota wa muziki wa Pop George Michael amefariki dunia jana baada ya moyo wake kushindwa kufanya kazi akiwa nyumbani kwake huko Oxfordshire Uingereza.

Mwanamuziki huyo aliyeanza muziki katika miaka 80, na kupata mafanikio zaidi akiimaba peke yake nje ya bendi, amefariki dunia kwa amani jana siku ya Krismasi, kwa mujibu wa msemaji wake.

Mwanamuziki mwenzake wa zamani wa bendi ya Wham! Andrew Ridgeley amesema amevunjika moyo kuwa kumpoteza rafiki yake kipenzi.
           George Michael akiwa na Andrew Ridgeley wakiimba pamoja na bendi ya Wham !
Picha hii inaaminika kuwa ni picha ya mwisho kupiga George Michael hii ilikuwa Septemba mwaka huu akipata mlo wa usiku na rafiki yake

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni