Bi. 
Janet Sosthenes Mwenda (wa pili kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa kituo
 cha Watoto Wetu Tanzania, Bw. Evans Tegete moja ya vitu 
vilivyowasilishwa kwenye kituo hicho ndoo ya sabuni ya unga. Kushoto ni 
Muhamasishaji na mchangishaji fedha wa “Mentoring and Networking”, Bi. 
Mary Sanga na wengine wanaoshuhudia ni watoto wa kituo hicho. (Picha 
zote na Andrew Chale, Modewjiblog).
Mmiliki
 na Mwendeshaji wa kipindi cha ‘Ongea na Janet’ Bi. Janet Sosthenes 
Mwenda ambaye pia ni mmiliki wa programu maalum ya vipindi vya watoto 
katika kutoa elimu katika televisheni kiitwacho ‘Tuwalinde Watoto Wetu’ 
kwa kushirikiana na marafiki zake wa kundi la “Mentoring and Networking”
 kupitia mitandao ya kijamii wametoa misaada mbalimbali ya vyakula na 
vinywaji kwa kituo cha Watoto Wetu Tanzania.
Akizungumza
 wakati wa kutoa misaada hiyo mapema jana 17 Januari, wakati wa tukio 
hilo lililofanyika kwenye kituo hicho kilichopo Kimara jijini Dar es 
Salaam, Janet Mwenda ambaye aliambatana na baadhi ya marafiki zake hao 
wa “Mentoring and Networking” wameweza kutoa misaada hiyo ya vyakula, 
vinywaji ambavyo vitasaidia kituo hicho.
“Kwa 
kuja hapa kutoa msaada huu ni kutokana na kuguswa na hali ya watoto 
wanaolelewa hapa na kwingineko kote. Naamini msaada huu utasaidia watoto
 wetu hapa kituoni naamini kwa hiki kidogo kitasaidia kwa siku kadhaa” 
alieleza Janet Mwenda.
Janet 
Mwenda ameongeza kuwa, amekuwa akifikiria zaidi kutoa misaada hivyo 
kufika hapo ni kutokana na kuguswa kwake kwa muda mrefu na amekuwa pia 
akitembelea kituo hicho kipindi cha nyuma hivyo kuwa miongoni mwa 
wanafamilia.
Kwa 
upande wake Muhamasishaji na mchangishaji fedha wa “Mentoring and 
Networking”, Bi. Mary Sanga ambaye aliambatana na Janet Mwenda katika 
kituo hicho ametoa wito kwa jamii kujitokeza kusaidia watoto wanaolelewa
 kwenye vituo kama hivyo na kuchangia chochote walicho nacho.
Pia 
amepongeza watu mbalimbali kwa kuguswa na hali ya watoto wanaolelewa 
kwenye vituo hivyo ameomba waendelee kujitokeza zaidi pindi wanapoguswa 
na masuala ya kusaidia jamii isiyo jiweza.
Naye 
Mkurugenzi wa kituo hicho, Ndugu Evans Tegete akitoa neno la shukrani 
mara baada ya kupokea msaada huo ambapo alishukuru kwa kuguswa kwa Janet
 Mwenda na marafiki zake kwani hadi sasa kituo hicho hakina Mfadhili wa 
kudumu zaidi wakitegemea kuendesha kituo kwa michango ya misaada ya watu
 mbalimbali wanaofika kituoni hapo.
“Tunashukuru
 kwa msaada huu. Kwani ni mkubwa sana na utasaidia kuendesha kwa siku 
kadhaa ndani ya kituo chetu. Kituo chetu kwa sasa tuna watoto na vijana 
zaidi ya 89 wakiwemo wale wanaosoma shule za Bweni na wa kutwa ambao 
wapo hapa kituoni.” Alieleza Mkurugenzi huyo.
Pia 
alieleza kuwa changamoto mbalimbali zinawakabili ikiwemo suala la ada za
 shule kwa watoto na vijana waliochini ya kituo hicho.
Kituo 
hicho kinacholea Watoto na vijana wa mitaani na wanaoishi katika 
mazingira magumu kina jumla ya watoto pamoja na vijana 120 kilianzishwa 
mnamo mwaka 1998 Kwa lengo la kuwasaidia watoto waliokosa malezi na 
huduma mbalimbali za kijamii. Kituo hicho kinapatikana Kimara Suka 
pamoja na Kijiji cha Mazizini Msata wilayani Bagamaoyo kinakabiliwa na 
changamoto mbalimbali hivyo uongozi wa kituo hicho kinawaomba watu 
binafsi na wafadhili mbalimbali kujitokeza kuwasaidia pindi waguswapo.
Mkurugenzi
 wa kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Bw. Evans Tegete akizungumza na 
wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa kituo hicho.
Bi. 
Janet Sosthenes Mwenda (kushoto) akipata fursa ya kuwa na watoto 
wanaolelewa kwenye kituo hocho cha Watoto Wetu Tanzania, kulia kwake ni 
Mary Sanga kutoka kundi la marafiki wa “Mentoring and Networking”.
Muhamasishaji
 na mchangishaji fedha wa “Mentoring and Networking”, Bi. Mary Sanga 
akitoa nasaha na kushukuru wale wote walioguswa kwa kuchangia mpango 
huo.
Bi. Janet Sosthenes Mwenda akipata fursa ya kuwa na watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho cha Watoto Wetu Tanzania.
Bi. 
Janet Sosthenes Mwenda akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) ambapo
 ameiomba jamii kuwa na tabia ya kusaidia jamii isiyojiweza ikiwemo 
watoto wanaolelewa kwenye vituo.
Binti 
Cecilia Sospita anayelelewa kwenye kituo hicho cha Watoto Wetu Tanzania,
 akishukuru kwa niaba ya watoto wenzake wanaolelewa kituoni hapo kwa 
msaada uliowasilishwa na Bi. Janet Mwenda.
Msaada uliotolewa kusaidia kituoni hapo.
Kijana Samson Furgence akishukuru kwa niaba ya watoto wenzake wa kituo hicho.
Zoezi la utoaji wa zawadi likiendelea.
Watoto
 na vijana wanaolelewa katika kituo hicho. Wengine ni wageni wa 
kujitolea "Volunteer" wa kituo hicho kutoka nchini Ujerumani wakiwa 
pamoja na watoto hao kituoni hapo.
Muhamasishaji na mchangishaji fedha wa “Mentoring and Networking”, Bi. Mary Sanga akitoa msaada katika tukio hilo.
Baadhi ya watoto na walezi wao wakifuatilia shughuli hiyo.
Janet Mwenda akishukuru watu mbalimbali kwa kumtia moyo katika kufanikisha shughuli hiyo.
Baadhi ya watoto hao.
Baadhi ya watoto hao.
Sala 
maalum ya kuombea vitu hivyo vilivyoletwa kituoni hapo pamoja na Baraka 
kwa waliofanikisha ikitolea na mmoja wa watoto wa kituo hicho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni