SSRA YAWAZINDUA WAJASIRIAMALI KUHUSU KUJIUNGA NA KUJIWEKEA AKIBA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII

Afisa Uhusiano wa Mamaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Agnes Lubuva (kushoto), akiwapatia maelezo wananchi pamoja na wajasiriamali kuhusu kazi na majukumu ya taasisi hiyo kwa jamii, walipotembelea banda hilo, wakati wa maonesho ya Wiki ya Fursa za Kifedha na Uwekezaji viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika, akitoa somo juu ya umuhimu wa kujiunga na kujiwekea akiba kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kwa manufaa ya baadaye ya familia, wakati alipokuwa akitoa elimu kwa wajasiriamali kutoka sehemu mbalimbali katika Wiki ya Fursa za Kifedha na Uwekezaji, viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.
Wajasiriamali kutoka sehemu mbalimbali jijini Dar es Saaam, wakimsikiliza Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika, alipokuwa akitoa elimu kuhusu, Umuhimu wa kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii, wakati wa Wiki ya Fursa za Kifedha na Uwekezaji, viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Sarah Kibonde Msika, akitoa somo kwa wajasiriamali juu ya umuhimu wa kujiunga na kujiwekea akiba kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii kwa manufaa ya sasa na baadaye ya familia, wakati wa Wiki ya Fursa za Kifedha na Uwekezaji, viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.
Wajasiriamali wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Sarah Kibonde Msika (hayupo pichani) katika Wiki ya Fursa za Kifedha na Uwekezaji, viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Wajasiriamali wakiwa makini wakimsikiliza Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Sarah Kibonde Msika, alipokuwa akitoa elimu kuhusu, Umuhimu wa kujiunga na kujiwekea akiba katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa manufaa ya baadaye na wakati matatizo,katika maadhimisho ya Wiki ya Fursa za Kifedha na Uwekezaji, viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Sarah Kibonde Msika, akitoa somo kwa wajasiriamali.
Wajasiriamali wakiwa katika kongamano la Wiki ya Fursa za Kifedha na Uwekezaji, ambapo walielezwa kuhusu umuhimu wa kujiunga na kuweka akiba zao katika mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa manufaa ya sasa na baadaye na Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Sarah Kibonde Msika (hayupo pichani), viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni