Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January 
Makamba akitia saini kitabu cha Wageni alipotembelea Kata ya Mbweni 
iliyopo Manispaa ya Kinondoni kwa ajili ya shughuli za upandaji mikoko 
katika eneo hilo.
    Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January 
Makamba akipanda mti aina ya mkoko katika fukwe za bahari ya hindi 
katika eneo la Mbweni jijini Dar es Salaam. Upandaji huo wa mikoko ni 
katika kuadhimisha wiki ya mazingira duniani, ambayo kilele chake ni 
kesho
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba  akishirikiana kupanda miti ya mikoko na wakazi wa kata ya  Mbweni jijini Dar es Salaam ikiwa ni kuelekea kilele cha siku ya mazingira hapo tarehe 5 juni.
 .
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. 
January Makamba akifurahia jambo na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbweni 
ambao walijumuika pamoja naye kupanda mikoko katika fukwe za Mbweni 
jijini Dar es salaam.
Waziri
 wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January 
Makamba akiongea na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) mara baada ya 
kumaliza kupanda mikoko katika fukwe za bahari ya Hindi katika kata ya 
Mbweni.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba Ametoa wito kwa Wananchi  wa
 Kata ya Mbweni kutunza mazingira na kutoa kipaumbele kwa mazingira. 
Aliyasema hayo wakati wa zoez la upandaji mikoko lilifanyika katika 
fukwe za bahari ya Hindi zilizoko Mbweni.
Akiongoza
 Wananchi wa Kata hiyo kupanda miche 5,000 ya mikoko , Waziri Mkamba 
alisititiza pia Wanafunzi wa shule waliopo katika eneo hilo kupenda 
mazingira yao na kuyatunza ili yawafae baadaye.
Wakisoma Risala yao , Wanawake wa Mbweni walimuomba Waziri awasaidie kuwapatia vitendea kazi  kwa
 ajili ya kuhudumia mikoko pamoja na kumuomba awasaide kuwatatulia 
changamoto wanazokutana nazo. Ikiwamo ya maafisa wa TRA kukata hovyo 
mikoko wanapokua wanafanya doria katika fukwe zaMbweni.
Mwisho
 Waziri aliwahukuru Wananchi wa Mbweni waliojitypkeza kujumuika naye 
katika zoezi hilo la upandaji mikoko. Shuhuli za upandaji mikoko ni 
kuelekea maadhimisho ya siku ya mazingira ambayo kilele chake ni tarehe 5
 juni kila mwaka. 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni