MOHAMMED ALI AFARIKI DUNIA

Mkali wa masumbwi duniani, Mohammed Ali akimuangalia George Foreman akiwa chini baada ya kumpiga sumbwi lililomwangusha katika raundi ya nane katika pambano lililofanyika mwaka 1974 Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo zamani ikiitwa Zaire.

Bondia Mohammed Ali, wa Marekani amefariki leo asubuhi akiwa na umri wa miaka 74.

Ali ambaye alhamisi alikimbizwa hospitali kwa matibabu, alikuwa na matatizo ya kupumua, hali ambayo ilitatanishwa zaidi na maradhi ya Parkinson, ambayo ni hali ya mgonjwa kutetemeka kila mara.

Alifariki katika jiji la Phoenix Arizona
Mohammad Ali akimpongeza mtoto wake Laila baada ya kushinda pambano lake la masumbwi. Laila alifuata nyayo za baba yake

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni