Mkurugenzi
 wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano akimuonesha Waziri 
wa Habari, Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye  baadhi ya wachezaji
 wa timu ya taifa chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys 
waliopatiakana kupitia michuano ya Airtel Rising Stars wakati wa 
uzinduzi wa awamu ya sita ya michuano hiyo uliofanyika Dar es Salaam 
Jumapili Juni 26 2016.
 Waziri
 wa Habari, Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akipinga mpira 
kuashiria uzinduzi wa rasmi wa michuano ya Airtel Rising Stars 2016. 
Uzinduzi huo umefanyika Jumapili 26 Juni 2016 kwenye makao makuu ya 
Airtel Tanzania Dar es Salaam.
 Waziri
 wa Habari, Utamanduni ,Sanaa na Michezo Nape Nnauye akisisitiza jambo 
wakati wa ufunguzi wa michuano ya Airtel Rising Stars 2016 jijini Dar es
 Salaam.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano akiongea wakati wa uzinduzi wa msimu wa 6 wa Airtel Rising Stars.
 Rais wa TFF Jamal Malinzi akiongea wakati wa uzinduzi wa msimu wa 6 wa Airtel Rising Stars.
 Waziri
 wa Habari, Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye akiwa katika picha 
ya pamoja na viongezi wa TFF pamoja na Airtel Mara baada ya uzinduzi wa 
Msimu wa sita wa michuano ya Airtel Rising Stars
Wafanyakazi
 wa Airtel wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, 
Utamanduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye wakati wa uzinduzi wa wa Msimu 
wa sita wa michuano ya Airtel Rising Stars.
Airtel yazindua msimu wa 6 wa michuano ya Airtel Rising Stars 2016
Dar es
 Salaam, Jumapili 26 Juni 2016  Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na 
Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye leo amezindua msimu wa sita wa mashindano
 ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars na 
kuwapongeza Airtel Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono juhudi 
zinazofanywa na Serikali pamoja na shirikisho la mpira wa miguu nchini 
(TFF) za kukuza mchezo wa soka.
“Programu
 za soka za vijana ndiyo muhimili wa maendeleo ya soka popote pale 
duniani. Ndiyo maana nasisitiza umuhimu wa mashindano ya Airtel Rising 
Stars ambayo matunda yake yameonekana dhahiri katika kipindi cha miaka 
mitano iliyopita”, alisema Nnauye.   
Alitoa
 mfano wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 Serengeti 
Boys ambayo wachezaji wake 10 wa kutumainiwa wametokana na Airtel Rising
 Stars. “Matunda ya Airtel Rising Stars vilevile yanaoneka dhahiri 
kwenye timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars ambayo wachezaji wake wote 
wanatokana na programu hii ya vijana”, alisema Nnauye. Klabu za daraja 
la kwanza na ligi kuu Tanzania bara pia zinafaidi matunda ya Airtel 
Risings Stars. 
Waziri
 amewataka viongozi wa soka kusimamia vizuri pragarmu ya Airtel Rising 
Stars ili kuweza kubaini vipaji vingi zaidi kupitia mashindano haya ya 
vijana ya kila mwaka yakishirikisha timu za wasichana na wavulana 
kuanzia ngazi ya mkoa na kuhitimishwa kwa fainali ya Taifa jijini Dar es
 Salaam.
Akizungumza
 katika hafla hiyo ya uzinduzi, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel 
Tanzania Beatrice Singano alimhakikishia waziri kuwa kampuni ya Airtel 
Tanzania ina nia thabiti ya kuendelea kudhamini michuano hiyo ambayo 
imesaidia kuzalisha wachezaji wengi chipukizi hivyo kuendeleza mchezo 
huo marufu hapa nchini.
Alisema
 Airtel Rising Stars mwaka inafanyika chini ya mwanvuli wa kampeni ya 
Airtel RURSA iliyozinduliwa mwaka jana kwa lengo la kuwahamasisha vijana
 kutumia fursa mbalimbali walizonazo ili kujiendeleza kiuchumi. “Airtel 
Rising Stars yenyewe ni Airtel FURSA kwa kuwa inawawezesha vijana 
kutumia vipaji vyao kujikwamua kimaisha kupitia mpira. Mpira ni chano 
cha kipato cha kuaminika”, alisema.
“Kwa 
kuwa na wateja wengi nchi nzima Tanzania bara na Zanzibar, Airtel 
Tanzania tunawiwa kuendelea kutoa sehemu ya faida yetu kwa jamii kupitia
 mchezo wa mpira wa miguu ambao ni marufu kuliko michezo yote hapa 
Tanzania. Ni njia ya kuwashukuru wateja wetu kwa kuedelea kutuunga 
mkono”, alisema.  
Kwa 
upande wake, Rais wa TFF Jamal Malinzi alisema programu ya Airtel Rising
 Stars imeleta mapinduzi na kubadilsha kabisa sura ya mchezo wa soka 
hapa nchini. “Nawapongeza Airtel Tanzania kwa kuendelea kutuunga mkono. 
Naamini kwamba tutapata mafanikio makubwa zaidi siku za usoni”, alisema.
Airtel
 Rising Stars mwaka huu itashirkisha timu kutoka mikoa ya Mwanza, 
Morogoro, Mbeya, Temeke, Ilala, Morogoro (wavulana) wakati mikoa 
itakayoshirikisha timu za wasichana ni Ilala, Kinondoni, Temeke, 
 Arusha, Lindi na Zanzibar.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni