Mkuu
 Wa Wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Hemed Mwanga akizungumza na wananchi
 (hawapo pichani) katika siku ya Kimataifa ya Kupiga Vita Matumizi 
Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa wa Pwani kulia ni Mkuu wa Kituo 
 cha Life and Hope Bagamoyo Sober House,Al-Kareem Bhanji.
 Mkuu
 Wa Kituo  cha Life and Hope Bagamoyo Sober House, Al-Kareem Bhanji aki 
akizungumza na wananchi (hawapo pichani) waliofika kwenye siku ya 
Kimataifa ya Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa 
wa Pwani kushoto ni Mkuu Wa Wilaya ya Bagamoyo,Alhaj Majid Hemed Mwanga.
 Wananchi
 wakifatilia mada mbalimbali  kwenye siku ya Kimataifa ya Kupiga Vita 
Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa wa Pwani.
 Waathirika wa Dawa za Kulevya akiandamana siku ya Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya, jana Mkoa wa Pwani.
 Maandamano yakeendelea.
 Kikundi cha Sana cha Bagamoyo wakiigiza kama Waathirika wa Dawa za Kulevya.
 Mkuu Wa Wilaya ya Bagamoyo,Alhaj Majid Hemed Mwanga akiwa kwenye picha ya  Waathirika wa Dawa za Kulevya.
Mkuu Wa Kituo  cha Life and Hope Bagamoyo Sober House,Al-Kareem Bhanji  akiwa kwenye picha ya  Waathirika wa Dawa za Kulevya
(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii)
Na Bakari Madjeshi,Globu ya Jamii
Kituo 
cha Usaidizi Wa Watu walioathirika na Dawa za Kulevya cha Life and Hope 
Bagamoyo Sober House leo,June 26,2016 kimeadhimisha siku ya Kimataifa ya
 Kupiga Vita Matumizi Mabaya ya Dawa za Kulevya.
Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka June 26 lakini kwa Mwaka huu Kituo cha Sober kimeadhimisha siku hiyo Wilayani Bagamoyo.
Akizungumza
 katika Maadhimisho hayo,Mkuu Wa Wilaya ya Bagamoyo,Alhaj Majid Hemed 
Mwanga amesema vita vya Mapambano ya Dawa za Kulevya si vya Serikali 
pekee wala vya mtu mmoja bali ni vita vya kila mtu,ambaye anapaswa 
kuwajibika katika eneo husika ili kutokomeza kabisa uingizwaji Wa Dawa 
hizo.
Pia,Mkuu
 huyo Wa Wilaya ametoa wito kwa Viongozi Wa Dini ,Wananchi pamoja na 
Vyombo vya Ulinzi na Usalama kushirikiana kwa pamoja katika kutoa 
taarifa za kuwafichua waingizaji Wa Dawa hizo ili Serikali kuwachukulia 
hatua kali za kisheria.
Amesema,Serikali
 imeahidi kupatikana kwa eneo kubwa ili kuendeleza kituo hicho na 
kuwasaidia vijana ambao ndio waathirika wakubwa Wa janga hilo na kuitaka
 jamii kuwatambua na kuwabaini waathirika wa Dawa hizo.
Kwa 
upande wake,Mkuu Wa Kituo hicho cha Life and Hope Bagamoyo Sober 
House,Al-Kareem Bhanji amesema kituo hicho kimesaidia watu zaidi ya 100 
mpaka sasa,ambapo ametoa Changamoto za ukosefu wa Majengo kituoni hapo 
 jambo ambalo limepelekea kwa sasa kulipa kodi kubwa ya pango.
Pia 
ameiomba Serikali kupatikana Ardhi ya kutosha ili kuweza kuongeza 
majengo na kukidhi haja ya kupokea Waathirika 200 ikiwa Wanaume 150 na 
Wanawake 50.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni