Katika
 kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli za kuhakikisha tatizo la 
madawati nchini linamalizika hadi kufikia Juni, 30 mwaka huu, Mkurugenzi
 Mkuu wa Mashirika ya IPP, Dk. Reginald Mengi ametoa msaada wa milioni 
70 kwa wilaya ya Handeni, Tanga na Bagamoyo, Pwani kila moja ikipata 
milioni 35 kwa ajili ya ununuzi wa madawati 1,000 ambayo yatasaidia 
kumaliza tatizo hilo katika wilaya hizo.
Akizungumza
 katika halfa ya kukabidhi pesa hizo kwa wakuu wa wilaya wa kampuni 
hizo, Dk. Mengi alisema ni muhimu kwa watanzania kuungana kwa pamoja na 
kusaidia kupatikana kwa madawati kwani kwa kufanya hivyo ni kulisaidia 
taifa.
Hata 
hivyo Dk. Mengi alisema kuwa anaamini kama watu matajiri nchini 
wakiungana kwa pamoja na kujadili jinsi ya kumaliza tatizo la madawati 
nchini basi jambo hilo litaweza kupatiwa ufumbuzi wa haraka tofauti na 
sasa ambapo linakwenda kwa mwendo wa kusuasua.
"Ukisaidia
 mtu mmoja katika elimu ni sawa umesaidia jamii na taifa kwa ujumla kama
 watu matajiri wakisema wakae kwa pamoja na kuangalia jinsi ya kumaliza 
tatizo hili linaweza kutatuliwa na shida ya madawati kumalizika.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akizungumza katika 
halfa ya kukabidhi milioni 70 kwa wilaya ya Handeni na Bagamoyo ambazo 
zitawezesha wilaya hizo kununua madawati 1,000 na kila wilaya kupata 
madawti 500.
"Matajiri
 wanatakiwa kutambua kuwa wanatakiwa kurudisha shukrani zao kwa Mungu, 
taifa na wananchi na hasa kwa walio na hali ya chini kwani hao ndiyo 
wanaowasaidia kufanya biashara zao kwa amani," alisema Dk. Mengi.
Aidha 
amewataka wakuu wa wilaya hizo kuondoa hofu ya kufukuzwa kazi kama 
watakuwa hawajakamilisha na wanachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuongeza 
juhudi huku akiwashauri kuandaa mikutano katika wilaya zao na 
kushirikisha wananchi wao ili waweze kuchangia na hatimaye tatizo hilo 
kumalizika.
Kwa 
upande wa mkuu w wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga na mkuu wa 
wilaya ya Handeni, Husna Rajab wamemshukuru Dk. Mengi kwa msaada ambao 
amewapatia na kuwataka watanzania wengine kuwa na moyo wa kujitolea kama
 jinsi amevyofanya Dk. Mengi kwa kuchangia upatikanaji wa elimu bora.
Awali 
kabla ya msaada ambao umetolewa na Dk. Mengi, wilaya ya Bagamoyo ilikuwa
 ikikabiliwa na upungufu wa madawati 2,463 na Handeni ikikabiliwa na 
tatizo la upungufu wa madawati 4,000.
Mkuu wa wilaya ya Handeni, Husna Rajab akizungumza katika halfa hiyo.
Mkuu 
wa wilaya ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga akizungumza katika halfa ya 
kupokea pesa kwa ajili ya madawati 500 yatakayokwenda katika wilaya yake
 kusaidia kupunguza tatizo la madawati.
Mkurugenzi Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akisaini mfano wa hundi kabla ya kuanza kuwakabidhi.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akimkabidhi mfano wa 
hundi ya milioni 35, Mkuu wa wilaya ya Haneni, Husna Rajab. Wa pili 
kushoto ni Mkurugenzi wa Mji wa Handeni, Kenneeth Haule, Mwenyekiti wa 
Mji wa Handeni, Twaha Mgaya na Mwenyekiti wa Halmshauri ya Handeni, 
Ramadhani Diliwa.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi akimkabidhi mfano wa 
hundi ya milioni 35 kwa ajili ya ununuzi wa madawati 500, Mkuu wa wilaya
 ya Bagamoyo, Alhaj Majid Mwanga. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi 
Chalinze, Edes Lukoa, Mkurugenzi wa Bagamoyo, Natujwa Melau, Mwenyekiti 
wa Halmashauri ya Bagamoyo, Ally Issa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya 
Chalinze, Said Zikatimu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni