Na  Mwandishi Maalum, New York
 Mkutano wa Tisa wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za
Watu  Wenye Ulemavu ( CRDP), umeanza jana
( Jumanne)  hapa Makao Makuu ya Umoja wa
Mataifa,  New York, Marekani.
Mada au  ujumbe wa
Mkutano huu wa siku tatu   ni “
Utekelezaji wa  Agenda  ya Maendeleo Endelevu ( Agenda 2030) Kwa Watu
Wote Wenye Ulemavu: Pasipo Kumwacha Yeyote”
Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania katika  Mkutano huu, unaongozwa na  Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Dr.
Abdallah Possi ( Mb). Wajumbe wengine ni Mhe. Riziki Lulinda ( MB), Mhe. Elly
Macha ( Mb) ,Mhe. Stella Ikupa ( Mb) , Bi Josephine Lyengi, Kaimu Kamishna
kuhusu watu wenye ulemavu na Bi. Ngusekela  Nyerere , Afisa Mambo ya Nje, Wizara ya Nje
na  Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Akizugumza  wakati wa
majadiliano ya  jumla mara baada ya  hafla ya ufunguzi , Naibu Waziri. Dr.
Abdallah Possi  amesema,   changamoto kubwa inayowakabilia watu wenye
ulemavu nchini Tanzania,  ni  fursa za kiuchumi.
“Licha
 ya 
mafanikio  kadhaa yakiwamo ya
utungaji wa sera,  sheria na  mabadiliko mbalimbali kuhusu  watu wenye 
ulemavu, bado kuna changamoto
nyingi ambazo zinatakiwa kufanyiwa kazi 
kwa lengo la kuwapunguzia matatizo watu wenye ulemavu  yakiwamo matatizo
 ya kutokuwa na fursa sawa  na kuondokana na umaskini”. Akaeleza
Naibu  Waziri
Na Kuongeza kwamba, Tanzania kama ilivyo kwa  nchi yingine inakabiliwa pia na vipaumbele
vinavyokinzana na ambavyo  ni muhimu
lakini    vikiwathiri zaidi watu wenye ulemavu.
Akavitaja baadhi ya 
vipaumbele hivyo kuwa  ni pamoja
na upatikanaji wa  maji safi na salama,  chakula, huduma za afya, elimu na ukosefu wa
ajiria.
Vile vile Naibu Waziri ameleza kuwa  mtazamo 
hasi kuhusu watu  watu wenye ulemavu
ni changamoto nyingine ambayo inatatiza ujumuishi wa watu wenye ulemavu katika
fursa  mbalimbali za  maendeleo ya kiuchumi na kijamii ambazo  wangeweza kunufaika nazo  bila ya kujali  hali zao.
Akizungumzia  
 kuhusu
mahitaji ya watu wenye ulemavu nchini Tanzania, 
Mhe. Dr. Possi, ameeleza washiriki wa mkutano huu kutoka nchi 164 ambazo
zimeridhia mkataba wa watu wenye ulemavu kwamba,  watu wenye ulemavu 
nchini  Tanzania wanakabiliwa na  tatizo kubwa la kutokuwa  vifaa 
saidizi ambavyo  vingewasaidia na
kuwawezesha   katika 
shughuli zao za kila siku.
Vivile akabainisha 
kuwa  mwaka  2015, Tanzania ilikuwa
moja ya wadhamini  wakuu wa Azimio kuhusu
watu wenye ualibino, azimio ambalo pamoja 
na mambo mengine limelenga katika kutafutia ufumbuzi baadhi ya
changamoto zimazowakabili  watu wenye
ualibino katika  maeneo mbalimbali
yakiwamo ya  elimu, afya na  ajira.
“ Bila ya kuwa na 
vifaa saidizi  watu wenye  ulemavu wa aina  yoyote ile wanashindwa  kupata fursa anuai ambazo kwayo
zingewawezesha kuishi  pasi  utegemezi na hivyo kuchangia katika yao
binafsi na maendeleo ya nchi  yao”
akasisitiza Naibu Waziri. Na akatumia fursa hiyo ya  kuhimiza upatikanaji wa vifaa saidizi kwa
watu wenye ulemavu ili wawe kujitegemea.
Awali 
 akifungua
mkutano  wa tisa  wa Mkataba wa Watu Wenye ulemavu,  Rais wa Baraza Kuu 
la  Umoja wa Mataifa,  Bw. Mogens Lykketoft, amesema nchi
ambazo  zimeridhia mkataba huo  zinaowajibu wa kuchukua hatua zote 
muhimu  zikiwamo za 
maendeleo jumuishi  kwa watu wenye
ulemavu.
“ Kila  nchi mwanachama
wa mkataba huu na asiye wamanachama anakazi ya kufanya, lakini katika
dunia  ya leo mafanikio hayamo  katika 
mikono ya serikali peke yake” akasisitiza Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa
Mataifa.
Na kwa sababu hiyo, ametoa wito kwa serikali zote pamoja na
wadau  mbalimbali kufanya kazi kwa
pamoja  kwa lengo la kuwawezesha  watu wenye ulemavu  zaidi 
ya  bilioni moja.
Pamoja
 na  hotuba   kutoka kwa 
nchi wanachama, mkutano huu ambao ni wa siku tatu  utakuwa na mijadala 
ya pembezoni  yenye mada tofauti. Mkutano huo pia  unashirikisha Asasi 
zisizo za kiserikali   zinazojihusisha na  masuala ya watu wenye 
ulemavu.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni