ONGEZEKO LA HATI FUNGANI LAATHIRI MAUZO YA HISA DSE

Meneja biashara na mauzo wa DSE Patrik Msusa akiongea na waandishi wa habari mapema leo.
Soko la hisa la Dar es Salaam –DSE limesema kuwa ongezeko la hati fungani katika soko hilo limetokana na baadhi ya wawekezaji kutafuta hathari ndogo zaidi za bei ya hisa.

Akizungumza na wanahabari jijinia na Dar Es Salaam meneja biashara na mauzo Patrick Msusa amesema kuwa hatua hiyo ya ongezeko la hati fungani limesababisha mauzo ya hisa katika soko hilo kushuka kutoka shs 13.2 bilion mpaka kufikia shs 8bilioni.

“hatua hii pia imeweza kusababisha makampuni matatu katika sekta ya mawasiliano kuingia katika orodha ya makampuni ya simu yaliorodhoshwa katika soko letu la hisa, ikiwemo Vodacom, Tigo na Airtel”. Alisema Patrick Msusa.

Vile vile ameongeza kwa kusema kuwa, katika takwimu za soko hilo kwa kipindi caha wiki sita zilizopita ukubwa wa mtaji wa makampuni ya ndani umeweza kupungua  kwa asilimia 2.4% wakati kampuni ya TBL ikiongoza kwa punguzo la asilimia 5% na sekta za kibiashara ikishuka kwa asilimia 15.6% ambapo hatua hiyo imetokana na kushuka kwa hisa za benk ya CRDB.

Hata hivyo aliyataka makampuni ya mawasiliano ya simu nchini kuweza kujiorodhesha kufuatia sheria ya serikali ya kuyataka makampuni hayo kuuza hisa za zao kwa wananchi kupitia soko hilo ili kukuza na kuchangia katika pato la taifa.
“Hadi sasa tunayo orodha ya makampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi matatu tu hivyo basi napenda kutoa wito kwa makampuni mengine kuweza kujiorodhesha katika soko letu”aliongeza Msusa.

Msusa aliongeza kuwa suala la kushuka kwa  mauzo ya hisa katika soko hilo limetokana na mdororo wa kiuchumi kwa siku za hivi karibu kuliyo yakumba baadhi ya makampuni hapa nchini.

Mwisho………………….

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni