JOE BIDEN AMTAKA RAIS MTEULE DONALD TRUMP KUACHA 'UTOTO'

Makamu wa rais wa Marekani Joe Biden amesema rais mteule Donald Trump anapaswa kukua, na amemkosoa kuhusiana na hatua yake ya kushambulia vyombo vya Kiitelijensia.

Kauli hiyo ya Bw. Biden, ameitoa huku Bw. Trump akitarajiwa leo kupata maelezo kutoka kwa vyombo vya kijasusi vya Marekani kuhusiana na madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa urais wa Marekani.

Bw. Biden amesema kwamba ni kutokuwa na akili kwa rais mteule kutokuwa na imani na vyombo vya Kiitelejinsia.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni