Mkurugenzi wa kampuni ya Econnet Hashim Magessa akiongea na wanahabari hawapo pichani leo jijini Dar es salaam kuzungumzia kampuni hiyo kuanzisha Kanzidata ya Elimu kuisaidia serikali kutatua cha
  
  
Mahmoud Ahmad Dar es salaam  
Tafiti
 zilizotolewa na bank kuu ya dunia kupitia delivery indicators 
imeonyesha kuwa 37% ya waalimu waliokutwa mashuleni hawakuwa madarasani 
katika muda wa masomo hali inayopelekea kushuka kwa viwango vya elimu 
nchini
  
Amesema hayo leo mkurugenzi mtendaji wa ECONNECT Bwn
 Hashimu Magesa alipokuwa akizungumza na wanahabari jijini dar es salaam
 leo,ambapo amesema kuwa jambo hilo la kukosekana kwa waalimu madarasani
 katika muda wa masomo linaashiria kuwa wanafunzi hawapati elimu kwa 
kiwango kilichokusudiwa na wizara ya elimu na mamlaka yake
  
Ameongeza
 kuwa pamoja na changamoto hizo za waalimu kumekuwepo na wanafunzi hewa 
pamoja na utoro uliopitiliza  hali inayopelekea kushuka kwa viwango vya 
elimu kwa kutokujua kusoma na kuandika
  
Aidha Bwn Magese 
amesema kuwa kutokana na changamoto hizo na nyinginezo zinazoikabioli 
sekta ya elimu hapa nchini ndio maana taasisi ya ECONNECT imekuja  na 
mfumo huo wa Kanzidata utakao isadia serikali kutatua changamoto za 
kielimu kwa ujumla
  
Amesema kuwa mfumo huo wa Kanzidata(DATABASE)utasaidia kuwa na takwim u sahihi zinazohusu kujua idadi shule,waalimu,wanafunzi,madarasa,madawati
 nk pamoja na mkwamo wa mawasiliano kati ya utawala wa shule na 
mzazi/mlezi utakaokuwa ukitoa taarifa kwa haraka juu ya maendeleo ya 
haki elimu kwa mwanafunzi kupitia mawasiliano ya simu za kiganjano ambao
 utagarimu shilingi mia tatu kwa ajili ya kupata huduma zote hizo
 
  
Bwn
 Magesa amesema kutokana na utafiti wa majaribio walioufanya kwenye 
wilaya ya ilala kwa jumla ya shule 152 ampo katika zoezi hilo 
waliorodhesha taarifa mbalimbali za kielimu kupitia takwimu sahihi 
ambazo kwa sasa zinawapa taarifa na kuokoa fedha ambazo zingetumika 
kuchapisha taarifa na huku taarifa hizo zikifika kwa haraka kwa wahusika
  
Hta
 hivyo taasisi ya ECONNECT imetoa wito kwa serikali kuutumia mfumo wa 
majaribio kwa ndani ya mwaka mmoja ili kujiridhisha na ufanisi wake,pia 
taasisi inawataka wadau mbali mbali wa elimu ikiwa ni pamoja na 
makampuni,taasisi na watu binafsi kushirikiana kwa pamoja kwaajili ya 
kuwezesha utekelezaji wa mfumo utakaosadia kuboresha elimu hapa nchini 
kwa manufaa ya taifa letu kwa ujumla.ngamoto za kielimu picha na mahmoud ahmad dar es salaam |   |   |   |   |   | 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni