Dar
 es Salaam. Vigogo wawili wa siasa za upinzani nchini, Edward Lowassa na
 Maalim Seif Sharif Hamad kesho watapanda jukwaani katika Skuli ya 
Fuoni, Zanzibar kumnadi mgombea ubunge Jimbo la Dimani kwa tiketi ya 
CUF, Abdulrazaq Khatib Ramadhan.
Katika
 Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Lowassa ambaye pia ni Waziri Mkuu wa 
zamani na Maalim Seif aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar 
katika Serikali iliyopita, waligombea urais wa Jamhuri ya Muungano na 
Zanzibar, mtawalia.
Uchaguzi
 huo wa Dimani, utafanyika Jumapili Januari 22, kujaza nafasi iliyoachwa
 na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Hafidh Ally Tahir aliyefariki dunia 
Novemba 11, mwaka jana katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Chini
 ya ushirikiano wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi 
(Ukawa), jana Chadema kilitangaza utaratibu jinsi vigogo wake 
watakavyoshiriki kampeni za uchaguzi huo kwa staili tofauti ili 
kuhakikisha mshirika wake CUF anaibuka kidedea.
Naibu
 Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu alisema jana kwamba kesho, 
Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu, atakuwa kiongozi wa kwanza 
wa Chadema kuhudhuria kampeni hizo akishirikiana na Maalim Seif ambaye 
pia ni Katibu Mkuu wa CUF.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni