WAUMINI WAFA KWA MOSHI WA MKAA WAKINGOJEA MWISHO WA DUNIA

Wafuasi watano wa dhehebu moja nchini Benin wamekufa kwa moshi wa mkaa, baada ya kuambiwa na kiongozi wao kuwasha moto katika chumba kilichofungwa wakiomba kungojea mwisho wa dunia.

Waumini kadhaa wa wamekimbizwa hospitali baada ya tukio hilo la mwishoni mwa wiki lililotokea katika mji wa Ajarra, karibu na Mji wa Porto Novo.

Waumini hao wa Kanisa Takatifu Mno la Yesu Kristo, kanisa lao limekuwa likiipinga dini ya Voodoo ambayo ndio dini kubwa kwa waumini wengi nchini Benin.

Waumini wa kanisa hilo lenye utata wamekuwa wakipambana na waumini wa madhehebu mengine nchini Benin.
                         Waumini wa Voodoo wakiwa katika maadhimisho ya siku ya imani yao

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni