Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya 
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati 
akifuatilia maelekezo yanayotolewa na mfanyakazi wa NHIF  alipotembelea 
 Taasisi hiyo leo jijini Dar es salaam, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi 
Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya nchini Bw. Bernard Konga.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya 
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa pili kulia 
akiangalia moja ya mafaili ya kuhifadhia kumbukumbu za madai katika 
ofisi za NHIF alipotembelea  Taasisi hiyo leo jijini Dar es salaam, wa 
kwabnza kulia ni  Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya nchini Bw. 
Bernard Konga.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya 
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa pili kulia 
akipata maelekezo kuhusu kitengo cha huduma kwa wateja kutoka kwa Mkuu 
wa kitengo hicho Bi. Anjela Mziray wa kwanza kushoto juu ya huduma 
zitolewazo na kitengo hiko alipotembelea NHIF leo jijini Dar es salaam, 
wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya nchini Bw. 
Bernard Konga.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya 
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile aliyesimama 
akiongea na watumishi wa Mfuko wa Bima ya Afya NHIF hawapo pichani 
alipotembelea  Taasisi hiyo leo jijini Dar es salaam, wa kwanza kushoto 
ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima ya Afya nchini Bw. Bernard Konga.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima 
ya Afya nchini NHIF Bw. Bernard Konga aliyesimama akiongea na watumishi 
wa taasisi hiyo hawapo pichani anayefuata aliyekaa ni Naibu Waziri wa 
Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile .
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Bima 
ya Afya nchini NHIF Bw. Bernard Konga aliyesimama akimuonesha Naibu 
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine 
Ndugulile baadhi ya tuzo walizopata katika kutoa huduma bora leo jijini 
Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya 
Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiangalia kitabu 
kinachohusu huduma za NHIF alichokabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko 
huo  Bw. Bernard Konga katikati wakati ziara yake katika taasisi hiyo 
leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya watumishi wa Mfuko wa 
Bima ya Afya nchini NHIF wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa 
Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile 
hayupo pichani wakati alipotembelea taasisi hiyo leo jijini Dar es 
salaam.
Picha na WAMJW
……………..
NA WAMJW-DAR ES SALAAM
MFUKO wa Bima ya Afya NHIF 
imetakiwa kufanya bidii katika kuongeza wanachama wa mfuko huo ili 
kufanya huduma za matibabu kupatikana kwa urahisi na gharama nafuu kwa 
watanzania wote.
Akizungumza na uongozi pamoja na 
watumishi wa Taasisi hiyo leo jijini Dar es salaam Naibu Waziri wa 
Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile 
amesema kuwa kuna umuhimu wa NHIF kuongeza wanachama wa mfuko huo.
“NHIF waweke uwezekano wa 
kuanzisha bima ya afya kwa wajawazito kwa bei nafuu hadi kufikia Julai 
2018 na pia huduma hii kuwa ya lazima kwa wananchi wote ili kuwasaidia  
kuepuka gharama kubwa za matibabu”  alisema Dkt. Ndugulile
 Aidha Dkt. Ndugulile alisema kuwa
 NHIF wanatakiwa kutengeneza mpango wa kuondoa adha kwa wagonjwa wenye 
kadi za bima za mfuko huo kunyanyapaliwa kwa kuwa hawana hela ya malipo 
papo hapo ili waweze kupata matibabu stahiki kwa wakati.
Kwa mujibu wa Dkt. Ndugulile 
amesema kuwa sio lazima wananchama wa mfuko huo wawe watumishi wa umma 
bali waangalie hata sekta binafsi ili kuweza kutoa huduma hiyo kwa 
maendeleo ya sekta ya afya nchini.
Mbali na hayo Dkt. Ndugulile 
amesema kuwa ili kuweza kufanikiwa kuondoa rufani za nje kunatakiwa 
kutengenezwa sheria ya kupandikiza viungo kama vile figo,moyo,vifaa vya 
usikivu  na vinginevyo ili kuleta mabadiliko katika sekta ya afya hivi 
sasa na miaka ijayo kwani wataalamu watazalishwa hapa nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa
 Mfuko wa Bima ya Afya nchini NHIF Bw. Bernard Konga amesema kuwa 
wamejidhatiti kuongeza wananchama wa mfuko huo kwa sekta mbalimbali na 
katika kutekeleza hilo wameanza mazungumzo na vyama vya ushirika ili 
kujua namna ya kuwasaidia wanachama wake.
“Tulishajipanga katika kutekeleza 
agizo hilo kwani mpaka hivi sasa tumeanza kuongea na vyama vya ushirika 
ikiwamo vyama vya wazalishaji korosho ili kuona uwezekano wa kuwasaidia 
katika kupata huduma hiyo” alisema Bw. Konga.
Aidha Bw. Konga amesema kuwa wapo 
bega kwa began a Seikali  katika kutekeleza sera ya afya kwa kutoa 
huduma ya kulipia matibabu kwa kila mtanzania aliyejiunga na mfuko huo  
ili kuweza kufikia malengo ya sera hiyo mpaka kufikia 2020.
Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya
 Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile leo alitembelea 
makao ya  Mfuko wa Bima  ya Afya NHIF na kuongea na Uongozi,watumishi 
pamoja na kutembelea sehemu ya kuhifadhia kumbukumbu za wadai,kituo cha 
huduma kwa teja na sehemu ya Tehama.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni