Mkuu 
wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Lughumbi ameipongeza Halmashauri ya Mji
 wa Geita kwa kusimamia vizuri fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa 
vilivyo chini ya mpango wa lipa kwa matokeo shule ya msingi Nguzo 
mbili. 
Akizungumza
 wakati wa ziara yake katika shule hiyo Mheshimiwa Robert Gabriel 
alisema kuwa ameridhishwa na kiasi cha fedha kilichotumika katika ujenzi
 wa madarasa kwa ubora wa hali ya juu katika shule hiyo. " Inashangaza 
sana kuona maeneo mengine wanatumia fedha zote kiasi cha shilingi 20 
milioni katika ujenzi wa darasa moja lakini kuna mapungufu mengi hivyo 
lazima kuwe na nidhamu ya matumizi ya fedha katika miradi ya 
Serikali"Alisema Lughumbi. 
Akiwa 
shuleni hapo Mkuu wa Mkoa ameagiza wakurugenzi kuunda na kutumia vikundi
 vya ujenzi vilivyo katika maeneo ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa 
madarasa pia kuishirikisha jamii ili kupunguza gharama kwa serikali na 
hatimaye fedha zinazobaki ziwezekufanya mambo mengine katika huduma za 
jamii. 
Mhandisi 
Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akiongozana na viongozi mbalimbali 
wa Mkoa wa Geita na Wilaya ya Geita wakati wa ukaguzi wa majengo 
yaliyotekelezwa kwa mpango wa lipa kwa matokeo Halmashauri ya Mji Geita.
Katika
 hatua nyingine Mhandisi Robert Gabriel aliutaka uongozi wa Shule ya 
Msingi Nguzo Mbili kusimamia suala la usafi na kumuagiza Mkurugenzi wa 
Halmashauri ya Mji wa Geita kuhakikisha anasimamia uimarishaji wa 
miundombinu hiyo ambayo mingine imeanza kupasuka. Aidha, ameagiza shule 
hiyo kupelekewa miundombinu ya maji ili vyoo vilivyojengwa vianze 
kutumika badala ya kufungwa.
Pamoja
 na kutembelea Shule ya Msingi Nguzo Mbili Mkuu wa Mkoa pia ameitembelea
 shule ya Sekondari na kukagua ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa 
vilivyojengwa kupitia mpango wa lipa kwa matokeo. Shule ya Msingi Nguzo 
mbili imejenga madarasa nane kwa kutumia shilingi milioni 13 kwa kila 
darasa, Ofisi 4, kisima cha maji na vyoo vya kisasa pamoja na ukarabati 
wa madarasa mengine katika shule hiyo kutokana na fedha iliyobaki katika
 bajeti ya darasa moja. 
Mkoa 
wa Geita una upungufu wa vyumba vya madarasa 8600 hivyo serikali 
imeandaa mpango kabambe wa kutokomeza tatizo hili kwa kushirikiana na 
jamii na wadau wote wa Mkoa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa.
Mhandisi
 Robert Lughumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita pamoja na viongozi wa Mkoa na 
Wilaya Geita na kamati ya usalama ya Mkoa  wakikagua miundombinu ya 
shule ya Msingi Nguzombili wakati wa ziara ya Mkuu huyo wa Mkoa 
Halmashauri ya Mji Geita.
Mhandisi
 Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akitoa maelekezo kwa Mkuu wa 
Wilaya ya Geita(Wakwanza kushoto) na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi 
Nguzombili wakati wa ziara yake katika Shule hiyo.
Mkurugenzi
 wa Halmashauri ya Mji Geita Mhandisi  Modest Apolinary  akifafanua 
jambo kuhusu utekelezaji miradi ya lipa kwa matokeo kwa Mkuu wa Mkoa 
wakati wa ziara yake shule ya msingi Nguzombili iliyopo Halmashauri ya 
Mji Geita.
 
Vyumba vya madarasa vilivyojengwa kupitia mpango wa lipa kwa matokeo Halmashauri ya Mji Geita. PICHA NA JUMAPILI MAGESA
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni