Nyumba iliyopo Bunju B ilivyokuwa kabla ya makabidhiano jana.
 Mkurugenzi
 wa Mkuu wa Global Group, Eric Shigongo (wa kwanza kulia) na George 
Majaba (wa pili kulia) pamoja na Meneja Mkuu wa Global, Abdallah Mrisho 
wakijadiliana jambo.
 ... Shigongo akizungumza machache mbela ya nyumba hiyo kabla ya kumkabidhi George Majaba jana.
 Mara baada ya kukata utepe, Shigongo akifungua nyumba hiyo.
 Ndani
 ya nyumba kushoto, George Majaba, Afisa Masoko, Jimmy Haroub, 
Mkurugenzi Mtendaji, Eric Shigongo, mke wa Majaba, Meneja Mkuu, Abdallah
 Mrisho na Mhariri Mwandamizi, Elvan Stambuli wakifurahia mandari ya 
nyumba.
 George Majaba akiwa na majirani zake wapya wa Bunju B kwenye nyumba yake mpya, hapo walikuwa wakimkaribisha.
 Majaba akizungushwa kuoneshwa mandari ya nje ya nyumba yake mpya.
Msafara
 wa magari ukiongozwa na pikipiki zaidi ya tano ulitokea makao makuu ya 
Global Group Sinza Mori Dar, huku Mshindi wa Shindano la Nyumba Awamu ya
 Pili, George Majaba akiwa kwenye gari la wazi aina ya BMW huku mke wake
 akiwa kwenye gari lingine na watoto wao . 
Msafara
 ulipita Barabara ya Shekilango, ukaingia Barabara ya Ali Hassani Mwinyi
 kisha ukaingia New Bagamoyo, njiani kwa kuwa kulikuwa na gari la 
matangazo, watu walikuwa wamejipanga kumshuhudi Majaba aliyejawa na 
tabasamu akipita akiwa kwenye gari hilo la wazi. 
 Msafara
 ulipofika Tegeta umati ulikuwa mkubwa na wengi waliokuwa wakimuona 
Majaba walikuwa hawaamini macho yao kwani yeye mshindi alikuwa 
akiwapungua mkono na msafara ukawa unaenda kwa mwendo wa polepole, hali 
iliyofanya baadhi ya wananchi kumkaribia mshindi na walisikika wakisema 
‘Hongera, Hongera!” Lakini abiria waliokuwa kwenye mabasi ya daladala 
nao walionekana wakitoa vichwa vyao madirishani na kumpongeza Majaba 
ambaye mara zote alikuwa na tabasamu usoni. 
 Hali
 ilikua hivyo hivyo msafara ulipofika Boko na baada ya kufika Bunju 
msafara ulisimama kabla ya kuingia Barabara ya Mabwepande ambapo kwa 
mwendo mfupi tu msafara uliingia kwenye nyumba mpya ya Majaba. Mara 
baada ya kufika, Meneja Mkuu, Abdallah Mrisho alitambulisha kwa wageni 
na wenyeji waliofika kushuhudia makabidhiano hayo na kisha akampa nafasi
 Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo kusema machache. 
“Kifupi leo tunamkabidhi nyumba yake Bwana Majaba. 
Ni
 jambo linalofurahisha kuona yupo hapa na familia yake ya mke na watoto 
watatu, hivyo bila kupoteza muda karibuni tufungue nyumba,” alisema 
Shigongo. Baada ya kusema maneno hayo Shigongo, Majaba na mkewe 
walishika utepe na Shigongo akaukata kuashirika kuwa sasa wamekabidhiwa 
nyumba yao. 
 Baadaye
 Majaba na watu wengine wakiongozwa na Shigongo waliingia ndani na 
kuoneshwa kila chumba, baadaye nje na uani ambako kulikuwa na nafasi 
kubwa na Shigongo alimuambia mke wa Majaba kwamba eneo hilo anaweza 
kufanyia miradi kama ya kufuga. Wenyeji walimkaribisha Majaba na baadaye
 wakapiga picha ya pamoja huku wakimpongesha kwa kushinda nyumba hiyo. 
Shughuli hiyo iliisha saa moja kasoro robo jioni. 
HABARI NA ELVAN STAMBULI, PICHA MUSSA MATEJA.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni