Naibu
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi Amina Shaban (kushoto) 
akiupokea ujumbe kutoka Umoja wa Ulaya, ukiongozwa na Kamishna wa 
Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo Bw. Neven Mimica (katikati) na 
Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania Bw. Roeland van de Geer, 
walipokuwa wanawasili Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam 
kwa ajili ya kutoa msaada wa Euro milioni 50 kwa Tanzania.
Ujumbe
 kutoka Umoja wa Ulaya pamoja na Maafisa wa Wizara ya Fedha na Mipango 
wakimsikiliza kwa makini, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. 
Doto James akitoa maelezo ya ujio wa ugeni huo kuwa ni neema kwa nchi ya
 Tanzania kwani Umoja wa Ulaya wametoa msaada wa Euro Milioni 50 
utasaidia vijijini 3600 nchini kupata umeme.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (kulia) na akimweleza
 jambo Kamishna wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Umoja wa 
Ulaya Mr. Neven Mimica wakati wa hafla fupi ya Umoja wa Ulaya (EU) 
kutiliana saini makubaliano ya msaada wa Euro milioni 50 kwa ajili ya 
kusaidia usambazi wa umeme vijijini kupitia Mradi Kabambe wa Kusambaza 
umeme Vijijini (REA).
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James akiwa pamoja na 
Kamishna wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Umoja wa Ulaya Bw. 
Neven Mimica wakisaini Mkataba wa msaada wa fedha za kusaidia usambazaji
 wa umeme Vijijini (EURO milioni 50) katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na
 Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James na Kamishna wa 
Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Umoja wa Ulaya Mr. Neven 
Mimica, wakibadilishana hati za makubaliano ya msaada wa ruzuku ya kiasi
 cha EURO Milioni 50 katika ukumbi wa wizara ya Fedha na Mipango, Jijini
 Dar es Salaam.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James akiwa na Ujumbe 
kutoka Umoja wa Ulaya pamoja na Maafisa waandamizi wa Wizara ya Fedha na
 Mipango wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kusaini mkataba wa 
msaada wa utekelezaji wa nishati ya umeme vijijini katika ukumbi wa 
Wizara ya fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James akiagana na Kamishna 
wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Umoja wa Ulaya Bw. Neven 
Mimica, baada ya kusaini mkataba wa msaada wa Euro milioni 50 ambazo 
Umoja huo umeipatia Tanzania kwa ajili ya kusambaza umeme vijijini 
kupitia Wakala wa Umeme Vijijini REA.
Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango
………………
Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
TANZANIA
 imezidi kupata neema kutoka Jumuiya ya Kimataifa ambapo Novemba 2, 
2017, Umoja wa Ulaya (EU) umeipatia Tanzania msaada wa Euro milioni 50, 
takriban Shilingi bilioni 130 kwa ajili ya kufadhili Mradi Kabambe wa 
Kusambaza Umeme Vijijini unaoendeshwa na Wakala wa Nishati Vijijini 
(REA).
Mkataba
 wa Makubaliano hayo umetiwa saini Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu 
Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto 
James na Kamishna wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Umoja wa 
Ulaya (EU) Bw. Neven Mimica.
Msaada
 huo umelenga kuwasaidia raia wa Tanzania kufikiwa na huduma nafuu ya 
nishati ya umeme kwa kupanua uwezo wa gridi ya Taifa pamoja na mtandao 
wa usambazaji umeme.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James ameushukuru Umoja wa
 Ulaya kwa msaada huo mkubwa utakaoiwezesha nchi kuwa na umeme wa 
uhakika utakaochangia ukuaji wa uchumi wa nchi na maendeleo ya watu 
wake.“Umoja
 wa ulaya ni wadau wetu muhimu wa maendeleo kutokana na misaada muhimu 
na mikubwa wanayotupatia, na kusadia agenda yetu ya maendeleo” alisema 
Bw. James
Alisema
 kuwa kiasi cha msaada wa Euro milioni 50 kilichotolewa na Umoja huo 
bila masharti yoyote si kidogo, na kwamba kitasaidia kutatua changamoto 
ya upatikanaji wa nishati ya umeme utakaochangia kuimarika kwa sekta ya 
viwanda itakayochochea ukuaji wa uchumi wa nchi.
Bw. 
Doto James alisema kuwa tangu Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini 
REA uanze miaka 9 iliyopita, idadi ya vijiji vilivyounganishiwa umeme 
imeongezeka kutoka vijiji 400 mwaka 2008 hadi kufikia vijiji 4395 hivi 
sasa.
Alisema
 kuwa ni matarajio ya Serikali kwamba ifikapo mwaka 2020, vijiji vyote 
12,000 hapa nchini vitakuwa vimeunganishwa na nishati hiyo hivyo 
kuchochea shughuli za uzalishaji viwandani na kiuchumi kwa wananchi, 
vitaimarika.
Kwa 
upande wake, Kamishna wa Ushirikiano wa Kimataifa na Maendeleo wa Umoja 
wa Ulaya (EU) Bw. Neven Mimica, amesema kuwa msaada huo wa Euro milioni 
50 wanaoutoa ni sehemu ya msaada wa Euro milioni 207 ambazo wanachama 
wengine wa Umoja huo, ikiwemo Sweden, Uingereza, Norway na Benki ya 
Dunia, watatoa kufanikisha mradi huo wa usambazaji umeme vijijini 
kupitia REA.
“Nguvu
 hizi za pamoja zitaviwezesha takriban vijiji 3,600 vilivyoko maeneo 
mbalimbali ya nchi ambapo watu zaidi ya milioni 1 wanatarajiwa kunufaika
 na mradi huo” Alisema Bw. Mimica.Alisema
 hatua hiyo itachangia kuimarika kwa ubora wa maisha ya wananchi wa 
Tanzania, kuimarika kwa sekta za afya, elimu na kuleta faida za kijamii 
na kiuchumi zinazoonekana kwao moja kwa moja hususan wanawake na watoto.
Misaada
 ya Umoja wa Ulaya kwa Tanzania imejikita katika Nyanja tatu za Utawala 
bora, Umeme na Kilimo endelevu ambapo Umoja huo kupitia Mfuko wake wa 
Maendeleo (EDF) umetenga kiasi cha Euro milioni 626 katika kipindi cha 
kuanzia mwaka 2014-2020

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni