Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu 
akisisitiza jambo mbele ya meza kuu na wageni wa alikwa, tukio 
lililojiri katika viunga vya Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi 
(TFDA).
 Watumishi
 wa umma na wageni waalikwa wakiwa wakifuatilia kwa ukaribu taarifa 
iliyokuwa ikiwasilishwa na Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu(MB) hayupo 
kwenye picha, mapema katika uzinduzi wa Maabara hamishika uliofanyika 
katika ofisi za TFDA.
 Waziri
 wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu 
akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maabara hamishika hizo, 
wakwanza kushoto ni mwakilishi kutoka WHO Dkt. Matthius Kamwa, watatu 
kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Bodi ya TFDA Bi. Zainabu na wa mwisho ni
 Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo Hiiti B. Sillo.
Mh.
 Ummy Mwalimu akipata maelekezo kuhusu Maabara hamishika hiyo wakati wa 
uzinduzi wa maabara hamishika mapema leo katika ofisi za Mamlaka ya 
Chakula, Dawa na Vipodozi wa kwanza kushoto ni mwakilishi kutoka WHO 
Dkt. Matthius Kamwa.
 Meza
 kuu ikiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na
 Watoto Mh. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa maabara hamishika mapema 
katika ofisi za Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Waziri
 wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu 
amesema kuwa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imekuwa ni Taasisi bora 
kwa Bara la Afrikakatika kudhibiti dawa na chakula ili watanzania wapate
 huduma bora.Ummy
 ameyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Maabara Hamishika jijini Dar es 
Salaam, amesema kuwa katika kulinda afya za  wananchi ni kupata dawa 
zinazostahili ambazo zimedhibitiwa na TFDA.Amesema
 kuwa matumizi ya dawa zisizo sahihi zinarudisha kasi ya uchumi ambayo 
inatokana na watu kuingia  gharama za kununua dawa hizo mara kwa mara na
 tatizo kubaki pale pale.
Ummy
 amesema kuwa licha ya kudhibiti dawa lakini TFDA isiwe kikwazo cha 
uwekezaji katika sekta ya viwanda ambapo wawekezaji wanatakiwa kufuata 
taratibu za nchi zilizowekwa.
Aidha
 amesema kuwa kazi ya TFDA ni kuhakikisha afya za wananchi zinalindwa 
kwa kuwa na wananchi wenye afya njema na wanaweza kuwfanya kazi na 
kuliletea Taifa maendeleo.
Amesema
 TFDA inatakiwa kuzingatia tathimini ya kina ya kisanyasi pamoja na 
matokeo ya uchunguzi wa maabara hivyo maabara  ya TFDA ni kiungo muhimu 
katika kutekeleza jukumu la kuhakikisha ubora na usalama wa bidhaa hizo.
Nae
 Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo amesema jukumu la TFDA ni 
kudhibiti ubora, usalama na ufanisi wa wa bidhaa ya chakula na dawa, 
vipodozi na vifaa tiba na vitandanishi ili kulinda afya ya jamii dhidi 
ya madhara yanayoweza kutokana na matumizi ya bidhaa duni na bandia.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni