Baada 
ya kupita miaka miwili bila kuchezwa kwa mashindano ya kuwania Kombe la 
Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki, michuano hiyo imerejea tena msimu
 huu na Tanzania imethibitisha kushiriki.
Nchi wanachama Tanzania Bara, Zanzibar, Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda, Somalia, Sudan, Sudan Kusini, Eritrea na Ethiopia.
Kaimu 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Kidao 
Wilfred amethibitisha kikosi cha kwanza cha ‘Taifa Stars’ kushiriki na 
matarajio ya kufanya vema michuano hiyo itakayofanyika kuanzia Novemba 
25, 2017 hadi Desemba 9, mwaka huu.
Kidao 
amesema kwamba uteuzi wa timu za kwanza kwa kila nchi mwanachama wa 
Baraza la Mpira wa Miguu la Afrika Mashariki ni makubaliano ya viongozi 
wa CECAFA waliokutana kwa pamoja huko Sudan, Septemba, mwaka huu.
Kutokana 
na makubaliano hayo ya kuita timu za kwanza, michuano hiyo itaathiri 
kidogot ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwa kuwa 
wachezaji wengi wanaounda kikosi hicho, wanatoka timu za VPL.
Mtendaji 
Mkuu wa Bodi ya Ligi (TPLB), Boniface Wambura amesema: “Tutakaa kama 
kamati na kuangalia siku ya Jumatano na Alhamisi baada ya michuano hiyo 
na kupanga ratiba ya mechi ambazo zitapanguliwa wakati wa michuano ya 
Chalenji.”
Mbali ya 
michuano hiyo, Tanzania imethibitisha kushiriki michuano ya Chalenji ya 
vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 itakayofanyika Bujumbura nchini 
Burundi kuanzia Desemba 12, 2017 hadi Desemba 22, mwaka huu.
Kadhalika,
 Tanzania imethibitisha kushiriki michuano ya Chalenji kwa wanawake 
ikienda kutetea taji katika michuano itakayofanyika Rwanda mwezi 
Desemba, mwaka huu. Tarehe rasmi itatajwa baadaye.
CECAFA 
imeamua kurejesha hadhi yake kwani mara baada ya michuano ya Chalenji ya
 vijana huko Burundi, mwakani itakuwa ni zamu ya Tanzania ambako 
michuano hiyo inatarajiwa kuanza Agosti 11, 2018 hadi Agosti 25, 
mwakani.
Wakati 
huo huo Kidao amethibitisha Tanzania kuwa wenyeji wa mashindano ya 
Vijana ya Chalenji ya CECAFA/CAF kwa vijana chini ya miaka 17 mwakani na
 mashindano hayo yatatumika kama sehemu ya kufanya maandalizi Fainali za
 Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 
(AFCON – U17).
Michuano 
ya mwakani ina baraka za Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa sababu 
shirikisho hilo linataka kutumia michuano hiyo ya vijana ya Kanda 
mbalimbali za Afrika kupata timu saba katika michuano AFCON – U17 ya 
mwaka 2019.
Kanda 
hizo ni CECAFA (Afrika Mashariki), COSAFA (Nchi za Kusini mwa Afrika), 
WAFU – UFOA (Afrika Magharibi); UNAF (Afrika Kaskazini) na UNIFFAC 
(Afrika ya Kati).

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni