NAIBU
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.
Hamisi Kigwangalla ameagiza kufungwa kwa Duka la dawa za binadamu la
Shine Care Pharmacy lililopo Temeke, baada ya kubainika kuendeshwa
kinyume cha sharia ikiwemo kutokuwa na kibali cha uendeshaji na mfamasia
husika.
Dk.
Kigwangalla ambaye aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya
Chakula, Dawa na Vipodozi, Mfamasia Mkuu wa Serikali pamoja na msajili
wa Baraza la famasia nchini na maafisa wengine, ambapo katika tukio hilo
mapema leo Februari 29.2016, walikuta madawa mbalimbali yaliyokwisha
muda wake na yale ambayo hayatakiwi kuuzwa katika duka kama hilo.
Aidha,
Dk. Kigwangalla akitoa agizo la kufungwa kwa duka hilo, ameagiza
kuchukuliwa hatua ikiwemo kupelekwa Mahakamani mara moja il iwe fundishi
na kwa maduka mengine yenye kufanya hivyo.
Kwa
upande wake, Mfamasia wa Serikali, Bw. Henry Irunde amebainisha kuwa,
dawa hiza za binadamu zilizokutwa hazifai kuuzwa katika maduka hayo na
pia duka ambalo linaendeshwa bila kuwa na Mfamasia ni kinyume na sharia
kwani watumiaji wakitumia dawa bila kuwa na maelezo ya kutosha kutoka
kwa mtaalam wa dawa zinaweza kusababisha usugu kwa mwili wa binadamu n
ahata kumsababishia matatizo.
Duka
hilo la dawa ambalo lipo hatua chacche kutoka Hospitali ya Temeke, ni
miongoni mwa maduka makubwa ya dawa za binadamu ambapo pia wachunguzi ha
wa madawa ya binadamu walibaini kuwa milango mingi zaidi kinyume na ile
inayotakiwa kuwa kwa maduka ya dawa hali ambayo walitilia mashaka
huenda vitendo vingine vya kutoa huduma vinatumika licha ya kuwa milango
hiyo ilifungwa kwa kile kilichoelezwa kuwa wahusika hawakuwapo.
Dk.
Kigwangalla amebainisha kuwa, zoezi hilo la kukagua maduka ya dawa ni
la nchi nzima na watazunguka nchi nzima kufanya ukaguzi huo bila kutoa
taarifa hivyo kwa yeyote atakaekutwa anaendesha kinyume cha sharia
atachukuliwa hatua stahiki.
Tazama tv, Kuona video hiyo hapa:
Imeandaliwa na Andrew Chal.
(Picha zote na Andrew Chale.)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni