Mkurugenzi
 wa Mipango miji na Vijiji Zanzibar Dkt. Mohammed Juma akizungumza kando
 ya Warsha ya kuanzisha kituo cha Mtandao wa Maeneo na mazingira ya 
Zanzibar huko Shangani mjini Zanzibar.
  Mwezeshaji
 wa mafunzo kutoka Taasisi ya Mazingira ya Finland Bi Riihz Teinirants 
akielezea hatua mbalimbali za kufuatwa kwa maafisa mbalimbali 
walioshiriki mafunzo ya kuanzisha kituo cha Mtandao wa Maeneo na 
mazingira ya Zanzibar huko Shangani mjini Zanzibar.  
 Picha
 no - 0707 na 0710 Baadhi ya Maafisa kutoka Zanzibar na wenzao wa 
Finland wakijadiliana namna ya bora ya kuanzisha kituo cha Mtandao wa 
Maeneo na mazingira ya Zanzibar katika ukumbi wa Hoteli ya Marumaru 
Shangani mjini Zanzibar.
Picha
 no - 0687 Maafisa kutoka Taasisi mbalimbali za Zanzibar wakisikiliza 
mafunzo yaliyokuwa yanatolewa na Maafisa kutoka Finland juu namna ya 
bora ya kuanzisha kituo cha Mtandao wa Maeneo na mazingira ya Zanzibar 
katika ukumbi wa Hoteli ya Marumaru Shangani mjini Zanzibar. 
Picha na Makame Mshenga
Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar.
IDARA
 ya Mipango miji na Vijiji Zanzibar kwa kushirikiana na taasisi 
mbalimbali za Zanzibar wanatarajia kuanzisha Kituo cha Mtandao wa 
Taarifa za Maeneo na mazingira ya Zanzibar ambapo Wananchi watalazimika 
kupata taarifa kupitia kituo hicho.
Taarifa
 hizo zitawekwa katika mfumo wa kidigitali na kuwekwa katika Mtandao huo
 ili kuepusha upotoshaji wa taarifa na pia zipatikane kwa wakati bila ya
 usumbufu.
Mkurugenzi
 wa Mipango miji na Vijiji Zanzibar Dkt. Mohammed Juma ameyasema hayo 
wakati wa warsha ya kuandaa utaratibu wa kuanzisha kituo hicho cha 
Mtandao Shangani mjini Zanzibar.
Amefahamisha
 kuwa kutokana na kuwepo kwa Vyanzo vingi vya Taarifa zinazohusu Maeneo 
ya Zanzibar kunapelekea baadhi ya Taarifa hizo kutokuwa sahihi na 
kupelekea mkanyiko katika jamii.
“Kwa
 sasa kuna Vyanzo vingi vya kujua maeneo na mazingira ya Zanzibar..kwa 
mfano ukienda kutaka taarifa juu ya eneo fulani inawezekana taarifa hiyo
 ikatofautiana na Vyanzo vingine lakini tutakapokuwa na Chanzo kimoja 
taarifa zitakuwa moja na sahihi”Alisema Dkt Mohamed.
Ametaja
 faida zitakazopatikana kupitia Mtandao huo kuwa nipamoja na 
kuwarahisishia Wananchi kupata taarifa popote walipo na kwa wakati 
kinyume na ilivyo sasa ambapo hulazimka kwenda katika Taaisi husika 
jambo ambalo huwaletea usumbufu.
Aidha
 amesema pia itakuwa ni sehemu ya uwazi kwa Serikali kupitia Taasisi 
zake ambapo kila kitu kitawekwa wazi na kupatikana kirahisi kupitia 
Mtandao huo.
“Mtandao
 huo utaweka wazi maeneo yote yakiwemo,Makaazi,maeneo ya 
uwekezaji..isipokuwa yale yakiusalama ili kumrahisishia mwananchi kuweza
 kupata Taarifa bila kuhangaishwa huku na kule” alibainisha Dkt 
Mohammed.
Aidha
 amebainisha kuwa katika Warsha ya kuandaa Mtandao huo Taasisi nane 
zimeshiriki ili kuwa na sauti moja juu ya maeneo na mazingira ya 
Zanzibar.
Amezitaja
 taasisi hizo kuwa ni pamoja na Mamlaka ya usimamizi wa ardhi, Idara ya 
Mazingira, Idara ya Misitu na maliasili zisizorejesheka na idara ya 
maendeleo ya uvuvi.
Taasisi
 zingine ni pamoja na Idara ya Rasilimali za baharini, Chuo kikuu cha 
taifa SUZA na Mamlaka ya Mazingira Zanzibar (ZEMA) ambazo zote 
zimeshiriki katika Mpango huo wa kuandaa Taarifa za pamoja.
Jumla ya shilingi Milion 140 zitatumika kuanzisha Kituo hicho cha Mtandao ambazo ni msaada kutoka Serikali ya Finland.
Kwa
 upande wake Mwezeshaji wa mafunzo kutoka Taasisi ya Mazingira ya 
Finland Bi Riihz Teinirants amesema Taasisi watendaji wa Taasisi hizo 
walioshiriki mafunzo wanajukumu la kuwafahamisha wenzao ili kutimiza 
lengo lililokusudiwa.
Aidha
 bi Riihz amesema mbali na kutoa mafunzo ya kuanzisha Kituo hicho cha 
Mtandao wataisaidia Zanzibar kutafuta taarifa za maeneo yake na kuziweka
 katika Kituo hicho hasa zile za mwambao wa bahari ili kuleta ufanisi 
unaohitajika.
Kunzishwa
 kwa kituo hicho cha Mtandao wa Taarifa za maeneo ya Zanzibar ni matokeo
 ya kukamilika kwa Mradi wa kutunza mazingira Zanzibar (SMOLE) 
uliofadhiliwa na Serikali ya Finland katika kuisaidia Zanzibar ambapo 
Mradi huo ulipata mafanikio makubwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni