
Mkurugenzi wa Uhamasishaji Biashara na Masoko wa Wizara ya Viwanda na Biashara Odilo Majengo akipokea maelekezo ya bidhaa kutoka kwa mwakilishi wa kampuni ya SLK Gold Taste wakati wa Mkutano na Maonyesho ya kibiashara ya kimataifa ya Mauritius jana
 Jijini Dar es Salaam. Wengine ni Mkurugenzi wa huduma za kibiashara wa 
Tantrade, Fidelis Mugenyi (kushoto) na Balozi wa heshima wa Mauritius, 
Abbas Rizvi. 
 Mkurugenzi
 wa Uhamasishaji Biashara na Masoko wa Wizara ya Viwanda na Biashara 
Odilo Majengo akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa Mkutano na Maonyesho ya kibiashara ya kimataifa ya Mauritius jana Jijini Dar es Salaam. Wengine ni Balozi wa heshima wa Mauritius, Abbas Rizvi (kulia) na Meneja wa kampuni ya Enterprise Mauritius, Rajen Subbamah,
 Meneja wa kampuni ya Enterprise Mauritius, Rajen Subbamah akizungumza wakati wa mkutano na maonyesho hayo
 Mkurugenzi wa TICC, David Lutabana akiongea wakati wa shughuli hiyo
 Baadhi ya washiriki wakifuatilia mkutano huo.
Washiriki wa maonyesho wakitembelea baadhi ya wafanyabiashara
Serikali
 imeahidi kuendelea kuboresha mazingira rafiki kwa wawekezaji ili 
kuongeza miradi ya uwekezaji ili kufikia lengo na Dira ya Tanzania kuwa 
nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.
Rai
 hiyo imetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara Bw. Charles Mwijage 
wakati wa ufunguzi wa Mkutano na Maonyesho ya kibiashara ya kimataifa ya
 Mauritius yakilenga kujenga mahusiano na kutizama fursa za kibiashara baina ya mataifa haya mawili jana Jijini Dar es Salaam.
Alisema
 moja kati ya jitihada zinazofanywa na serikali ni pamoja na matumizi ya
 teknolojia ya habari na mawasiliano kufanya baadhi ya mambo ambapo sasa
 usajili wa kampuni unaweza kufanywa mtandaoni.
“Natoa
 wito kwa ujumbe wa wafanyabiashara kutoka Mauritius kuwekeza nchini 
kutokana na uwepo wa rasilimali za kutosha, bandari pamoja na soko la 
uhakika kwani nchi yetu inapakana na nchi saba ambazo muwekezaji anaweza
 kuuza bidhaa huko kwa urahisi,” alisema Mh. Mwijage katika hotuba yake 
iliyosomwa naMkurugenzi wa Uhamasishaji Biashara na Masoko wa Wizara ya Viwanda na Biashara Odilo Majengo.
Maonyesho hayo yanaandaliwa na kampuni ya Talemwa Investment Consulting Company (TICC) pamoja na  Enterprise Mauritius kwa ushirikiano na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) na Chemba ya Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA).
Awali akiongea wakati wa mkutano huo, Mkurugenzi
 wa TICC, Bw. David Lutabana alisema maonyesho hayo ni fursa ya kipekee 
inayowakutanisha wafanyabiashara kutoka nchi hizi mbili ili kuweza 
kubadilishana uzoefu pamoja na kujadili fursa mbalimbali zilizopo katika
 nchi hizo.
Akizungumza
 wakati wa shughuli hiyo, Meneja wa kampuni ya Enterprise Mauritius, 
Rajen Subbamah, alisema sekta zinazoshiriki kutoka Mauritius ni pamoja 
na sekta ya ukandarasi, bidhaa za kilimo, kemikali, viwanda vya 
utengenezaji nguo na vidani, pamoja na sekta zingine.
“Nchi
 yetu ina uhaba mkubwa wa malighafi na kwa upande mwingine Tanzania 
imebarikiwa kwa kiasi kikubwa kuwa na rasilimali mbalimbali. Kupitia 
mkutano huu tunatizamia kujenga mahusiano na wafanyabiashara wa hapa 
Tanzania ili tuweze kufanya biashara zitakazonufaisha pande zote mbili,”
 alisema Bw. Subbamah.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni