Katibu Mkuu Ofisi ya Rais 
TAMISEMI  Mhandisi Mussa  Iyombe akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa 
Habari leo jijini Dar es salaam kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi na
 ukarabati wa barabara za Halmashauri nchini unaotekelezwa kwa 
ushirikiano na shirika la Maendeleo la Japan ( JICA) mradi unaolenga 
kuwajengea uwezo wahandisi wa Halmashauri na Mikoa katika kusimamia na 
kukarabati barabara zilizopo katika maeneo yao kwa kushirikiana na 
wananchi.
Mhandisi  wa Halmashauri ya 
Wilaya ya Chamwino Godwin Mpinzile akieleza kwa waandishi wa Habari 
kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara na ukarabati katika 
Halmashauri hiyo unaofadhiliwa na JICA ukilenga kuwashirikisha wananchi 
katika ujenzi na utunzaji wa barabara hizo ili ziweze kudumu
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais 
TAMISEMI  Mhandisi Mussa  Iyombe akimpongeza  Mwakilishi Mkazi wa 
Shirika la maendeleo la Japan (JICA) hapa nchini bw. Nagase Toshio kwa 
ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Japan hali iliyochangia 
kufanikiwa miradi ya ujenzi wa barabara katika halmashauri mbalimbali 
hapa nchini inayofadhiliwa na shirika hilo.
Muwakilishi Mkazi wa Shirika la 
maendeleo la Japan (JICA) bw. Nagase Toshio akifafanua kuhusu 
ushirikiano mzuri uliopo kati ya Serikali ya Tanzania na Japan katika 
kutekeleza mradi huo unaolenga kujenga uwezo kwa wahandisi wa 
Halmashauri hapa nchini ili waweze kuwashirikisha wananchi katika miradi
 ya barabara inayotekelezwa ili waweze kujiletea maendeleo .
Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya
 ya Iringa  bw. leopold  Runji akitoa ushuhuda wa namna halmashauri hiyo
 ilivyonufaika na mradi wa ujenzi na ukarabati wa barabara unaotekelezwa
 katika halmashauri  hiyo kwa ufadhili wa shirika la JICA.(Picha zote na
 frank Mvungi-Maelezo)
………………………………………………………………………………………………………….
Frank Mvungi-MAELEZO
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais 
TAMISEMI bw. Mussa Iyombe amewataka wananchi kutunza barabara 
zinazojengwa  na Serikali kwa kushirikiana na wafadhili katika 
Halmashauri zote hapa nchini.
Akizungumza leo Jijini Dar es 
salaam katika hafla fupi ya kupokea ripoti ya utekelezaji wa mradi wa 
Ujenzi na ukarabati wa barabara za halmashauri nchini  Iyombi 
amebainisha kuwa mradi huo umefadhiliwa  na  Shirika  la Maendeleo la 
Japan (JICA) .
“Mradi huu unatekelezwa katika Halmashauri  za Iringa,Mufindi,Chamwino na Kondoa” alisisitiza Iyombe.
Akifafanunua kuhusu utekelezaji 
wa mradi huo  Iyombe amebainisha kuwa  unadhamiria kujenga uwezo kwa 
wahandisi wa Mikoa na Halmashauri hapa nchini  ili waweze kushirikiana 
na wananchi katika kujenga  na kulinda miundo mbinu hiyo kwa maslahi ya 
Taifa.
 Aidha  Iyombi  amewata 
wakurugenzi wa Halmashauri  ambazo mradi huo unatekelezwa  kutunza 
barabara hizo ili zilete matokeo yaliyokusudiwa.
Akizungumzia ushirikiano mzuri 
uliopo kati ya Japan na Tanzania Iyombe amesema kuwa maeneo ambayo 
Tanzania imekuwa ikipata ufadhili kutoka Japan ni Sekta ya 
Kilimo,Viwanda,Uimarishaji wa Utawala bora.
Kwa upande wake mwakilishi mkazi 
wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) bw. Nagase Toshio amesema kuwa  
Shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika 
kutekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Mradi wa Ujenzi na Ukarabati wa 
barabara katika Halmashauri hapa nchini unatekelezwa kwa awamu ambapo 
awamu ya kwanza imekamilika katika Halmashauri za Chamwino na Iringa na 
awamu ya pili imekamilika katika Halmashauri za Kondoa na Mufindi ambazo
 ripoti ya utekelezaji wake iliwasilishwa leo katika mkutano wa siku 
moja ulifanyika Jijini Dar es salaam ukilenga kufanya tathmini ya 
utekelezaji kabla ya kuanza kwa awamu ya tatu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni