BIBI WA MIAKA 106 ATINGA IKULU KWA FURAHA NA MBWEBWE NA KUMSHANGAZA RAIS OBAMA


Hali ya hisia kali ilitawala katika Ikulu ya Marekani baada ya kibibi cha miaka 106 kutinga Ikulu kikiwa na furaha tele huku kikicheza na rais Barack Obama na mkewe Michelle, licha ya kuwa na umri mkubwa.

Kikongwe huyo machachari alipaza sauti kwa furaha mara tu ya kuingia Ikulu ya Marekani huku akimsalimia rais Obama na kisha kusema alifikiri asingewahi kuingia Ikulu katika maisha yake.

Bibi Virginia McLaurin alionekana kutimiza ndoto yake ya muda mrefu aliyokuwa akiiota alijawa na furaha isiyo na kifani na hakusita kusema kuwa anafuraha kushuhudia rais mweusi akiiongoza Marekani.
                              Bibi Virginia McLaurin akicheza muziki na Michelle Obama 
          Rais Obama akiangua kicheko wakati akicheza na bibi huyo pamoja na mkewe
                  Michelle Obama akimkumbatia kwa furaha Bibi Virginia McLaurin

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni