Baadhi ya waandaji wa Filamu 
nchini wakifuatilia mada katika kikao kilichowakutanisha waandaaji wa 
Filamu,Bodi ya Filamu, COSOTA na Kampuniya BORA PAMOJA LTD ili kujadili 
bidhaa ya Kampuni hiyo inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali 
ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza 
kazi zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu
 Tanzania Bibi. Joyce Fissoo akizungumza wakati wa kikao cha wasanii na 
Kampuni ya Bora Pamoja Ltd ili kujadili bidhaa yao ya Tazama Kidigitali 
ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu nchini 
kuusambaza Filamu zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es 
Salaam.A
fisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya 
BORA PAMOJA LTD Bi. Beatrice Pugwe akizungumza katika kikao 
kilichowakutanisha waandaaji wa Filamu na Kampuni yao ili kujadili 
bidhaa ya Kampuni hiyo inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali 
ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza 
kazi zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa 
Kampuni ya BORA PAMOJA LTD Bw. Mwanga Mwakibete akizungumza katika kikao
 kilichowakutanisha waandaaji wa Filamu na Kampuni yao ili kujadili 
bidhaa ya Kampuni hiyo inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali 
ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza 
kazi zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
Rais wa Shirikisho la Filamu 
Tanzania (TAFFA) Bw. Simon Mwakifamba akichangia mada katika kikao 
kilichowakutanisha waandaaji wa Filamu,Bodi ya Filamu, COSOTA na 
Kampuniya BORA PAMOJA LTD ili kujadili bidhaa ya Kampuni hiyo 
inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali ambayo inatoa fursa kwa 
watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza kazi zao kupitia mfumo wa
 kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
……………………………………………………………………………………………………
Na Shamimu Nyaki.
“Mmebuni wazo zuri lenye tija kwa
 waandaaji wa waongozaji wetu ambapo naamini itawaletea manufaa katika 
kazi zao wanazotengeza ili ziwe na faida kwao kwa kujitangaza kimataifa 
pamoja na kukuza kipato chao.’’ Alisema Bi Joyce.
Kampuni ya Bora Pamoja Limited 
imeanzisha mfumo mpya  wa usambazaji wa Filamu za hapa nchini kwa njia 
 ya kidigitali  ili kuweza kujitangaza kimataifa.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es 
Salaamu na  Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bi Beatrice Mpungwe alipokuwa 
anazugumza na waandaaji pamoja na  wasambazaji wa filamu za hapa nchini 
ambapo amesema kampuni hiyo itawawezesha  kukodisha filamu zao kwa 
wakati wowote wanaota pamoja na  kujitangaza kimataifa.
Bi Beatrice ameongeza kuwa  
kampuni hiyo ina nia ya kutangaza na kusambaza filamu kwa njia ambayo 
inaendana na wakati uliopo kwa kukuza kazi za watengenezaji na 
wasambazaji wa filamu  kwa ajili ya kuhifandhi kumbukumbu ya nchi na 
vizazi vijavyo.
‘’Mpango huu una nia ya 
kubadilisha jinsi tunavyoweza kutengeneza filamu zetu ziwe katika 
kiwango cha kimataifa kuanzia uandishi,uigizaji, uongozaji na 
utengenezaji”.Alisema Bi Beatrice.
Aidha  Katibu Mtendaji wa Bodi ya
 Filamu nchini Bi Joyce Fissoo ameipongeza Kampuni hiyo  na kuwashauri 
waandaaji na wasambazaji wote kujiunga na mfumo huo kwakua una lengo la 
kubadilisha uchumi na soko la kazi zao.
Amesema kuwa Mfumo huo 
utawawezesha kujua ni idadi ngapi ya filamu  zimeingia sokoni ambazo 
tayari zimeshafanyiwa uhakiki na Bodi ya Filamu ili kuweza kufikia lengo
 la kuinua tasnia ya filamu hapa nchini.
“Mmebuni wazo zuri lenye tija kwa
 waandaaji wa waongozaji wetu ambapo naamini itawaletea manufaa katika 
kazi zao wanazotengeneza ili ziwe na faida kwao kwa kujitangaza 
kimataifa pamoja na kukuza kipato chao.’’ Alisema Bi Joyce.
Hata hivyo mfumo huu utashawishi 
wawekezaji kutoka sehemu  tofauti ndani na nje ya nchi,kuwekeza katika 
vitendea kazi thabiti vitakavyosaidia katika kutengeneza kazi zenye 
ufanisi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni