Usambazaji mpya wa filamu kwa njia ya digitali Waanzishwa.


ws1
Baadhi ya waandaji wa Filamu nchini wakifuatilia mada katika kikao kilichowakutanisha waandaaji wa Filamu,Bodi ya Filamu, COSOTA na Kampuniya BORA PAMOJA LTD ili kujadili bidhaa ya Kampuni hiyo inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza kazi zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
ws2
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo akizungumza wakati wa kikao cha wasanii na Kampuni ya Bora Pamoja Ltd ili kujadili bidhaa yao ya Tazama Kidigitali ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu nchini kuusambaza Filamu zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.A
ws3
fisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya BORA PAMOJA LTD Bi. Beatrice Pugwe akizungumza katika kikao kilichowakutanisha waandaaji wa Filamu na Kampuni yao ili kujadili bidhaa ya Kampuni hiyo inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza kazi zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
ws4
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Kampuni ya BORA PAMOJA LTD Bw. Mwanga Mwakibete akizungumza katika kikao kilichowakutanisha waandaaji wa Filamu na Kampuni yao ili kujadili bidhaa ya Kampuni hiyo inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza kazi zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
ws5
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFFA) Bw. Simon Mwakifamba akichangia mada katika kikao kilichowakutanisha waandaaji wa Filamu,Bodi ya Filamu, COSOTA na Kampuniya BORA PAMOJA LTD ili kujadili bidhaa ya Kampuni hiyo inayojulikana kwa jina la Tazama Kidigitali ambayo inatoa fursa kwa watengenezaji na wamiliki wa Filamu kuusambaza kazi zao kupitia mfumo wa kidigitali leo jijini Dar es Salaam.
……………………………………………………………………………………………………
Na Shamimu Nyaki.
“Mmebuni wazo zuri lenye tija kwa waandaaji wa waongozaji wetu ambapo naamini itawaletea manufaa katika kazi zao wanazotengeza ili ziwe na faida kwao kwa kujitangaza kimataifa pamoja na kukuza kipato chao.’’ Alisema Bi Joyce.
Kampuni ya Bora Pamoja Limited imeanzisha mfumo mpya  wa usambazaji wa Filamu za hapa nchini kwa njia  ya kidigitali  ili kuweza kujitangaza kimataifa.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaamu na  Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bi Beatrice Mpungwe alipokuwa anazugumza na waandaaji pamoja na  wasambazaji wa filamu za hapa nchini ambapo amesema kampuni hiyo itawawezesha  kukodisha filamu zao kwa wakati wowote wanaota pamoja na  kujitangaza kimataifa.
Bi Beatrice ameongeza kuwa  kampuni hiyo ina nia ya kutangaza na kusambaza filamu kwa njia ambayo inaendana na wakati uliopo kwa kukuza kazi za watengenezaji na wasambazaji wa filamu  kwa ajili ya kuhifandhi kumbukumbu ya nchi na vizazi vijavyo.
‘’Mpango huu una nia ya kubadilisha jinsi tunavyoweza kutengeneza filamu zetu ziwe katika kiwango cha kimataifa kuanzia uandishi,uigizaji, uongozaji na utengenezaji”.Alisema Bi Beatrice.
Aidha  Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Bi Joyce Fissoo ameipongeza Kampuni hiyo  na kuwashauri waandaaji na wasambazaji wote kujiunga na mfumo huo kwakua una lengo la kubadilisha uchumi na soko la kazi zao.
Amesema kuwa Mfumo huo utawawezesha kujua ni idadi ngapi ya filamu  zimeingia sokoni ambazo tayari zimeshafanyiwa uhakiki na Bodi ya Filamu ili kuweza kufikia lengo la kuinua tasnia ya filamu hapa nchini.
“Mmebuni wazo zuri lenye tija kwa waandaaji wa waongozaji wetu ambapo naamini itawaletea manufaa katika kazi zao wanazotengeneza ili ziwe na faida kwao kwa kujitangaza kimataifa pamoja na kukuza kipato chao.’’ Alisema Bi Joyce.
Hata hivyo mfumo huu utashawishi wawekezaji kutoka sehemu  tofauti ndani na nje ya nchi,kuwekeza katika vitendea kazi thabiti vitakavyosaidia katika kutengeneza kazi zenye ufanisi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni