Katibu
 Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na watu wenye ulemavu Bw.
 Eric Shitindi akizungumza na vijana (hawapo pichani) alipokuwa 
akifungua kikao cha wadau wa maendeleo ya vijana katika kuchangia 
uandaaji wa kanuni za uendeshaji wa Baraza la Vijana Taifa jana jijini 
Dar es Salaam.
 Mkurugenzi
 Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi akizungumza wakati wa kikao cha 
wadau wa maendeleo ya vijana katika kuchangia uandaaji wa kanuni za 
uendeshaji wa Baraza la Vijana Taifa jana jijini Dar es Salaam.
 Mwezeshaji
 Bw. Patrick Kipangula (aliyesimama) akitoa mada kwa wadau wa maendeleo 
ya vijana wakati wa kikao cha kuchangia uandaaji wa kanuni za uendeshaji
 wa Baraza la Vijana Taifa jana jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe  wa
 maendeleo ya vijana akichangia mada wakati wa kikao cha kuchangia 
uandaaji wa kanuni za uendeshaji wa Baraza la Vijana Taifa jana jijini 
Dar es Salaam.
 Wawakilishi
 kutoka Mamlaka mbalimbali za Serikali, Asasi za kiraia, Vyama vya 
siasa, Taasisi za kidini, Vijana wenye ulemavu, Shule za sekondari na 
Shule za msingi wakifuatilia kwa makini mada zilizokua zikiendelea 
wakati wa kikao cha kuchangia uandaaji wa kanuni za uendeshaji wa Baraza
 la Vijana Taifa jana jijini Dar es Salaam.
 Katibu
 Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na watu wenye ulemavu Bw.
 Eric Shitindi (watatu kushoto waliokaa) katika picha ya pamoja na 
vijana wenye ulemavu wakati wa kikao cha kuchangia uandaaji wa kanuni za
 uendeshaji wa Baraza la Vijana Taifa jana jijini Dar es Salaam. Wapili 
kulia (waliokaa) ni Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi, 
wapili kushoto ni Mwenyekiti wa kikao Bw. Godwin Kunambi, na wanne kulia
 (waliosimama) ni Mkurugenzi msaidizi Vijana Bibi. Ester Riwa
Picha na: Genofeva Matemu - Maelezo
Na; Genofeva Matemu – Maelezo
SERIKALI
 imedhamiria kuhakikisha kuwa vijana wanakuwa na chombo chao chenye 
kujali utaifa, uzalendo na maslai bila kujali itikadi za kisiasa, 
kidini, rangi, hali za kiuchumi, jinsia na maumbile kwa kuandaa kanuni 
zitakazolifanya Baraza la Vijana Taifa kuwa huru na lenye haki.
Hayo
 yamesemwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na 
watu wenye Ulemavu Bw. Eric Shitindi alipokuwa akifungua kikao cha wadau
 wa maendeleeo ya vijana katika kuchangia uandaaji wa kanuni za 
uendeshaji wa Baraza la Vijana Taifa jana jijini Dar es Salaam.
“Nimuhimu
 kuunda Baraza kisheria litakalokuwa na uwakilishi wa vijana wa makundi 
yote ili liweze kutumika katika kuleta umoja na mshikamano wa kitaifa” 
alisema Bw. Shitindi
Aidha
 Bw. Shitindi amelipongeza Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa 
kuweza kutunga sheria Na. 12 ya mwaka 2015 ya Baraza la Vijana Taifa 
ambalo litaleta maendeleo ya vijana na nchi kwa ujumla.
Akizungumza
 katika kikao hicho mwenyekiti aliyeteuliwa kuongoza mjadala huo Bw. 
Godwin Kunambi amesema kuwa Vijana takribani 120 wamepata fursa adhimu 
ya kushiriki katika uandaaji wa kanuni za uendeshaji wa Baraza la Vijana
 Taifa hivyo kuwataka vijana hao kujadili mambo ya msingi 
yatakayowawezesha wananchi wa Tanzania hususani vijana kutatua kero zao 
kupitia Baraza hilo.
Naye
 mwakilishi kutoka kundi la watu wenye ulemavu Bw. Gaston Hemed Mcheka 
ameipongeza Serikali kutoa nafasi kwa kundi la watu wenye ulemavu kuwa 
na uwakilishi kuanzia ngazi ya kata hadi mkoa pindi Baraza la Vijana 
Taifa litakapoanza ambapo kundi hilo litatumia nafasi hiyo kutatua 
changamoto zinazowakabili.
Kikao
 cha wadau wa maendeleo ya vijana katika kuchangia uandaaji wa kanuni za
 uendeshaji wa Baraza la Vijana Taifa kimeshirikisha takribani vijana 
120 kutoka Mamlaka mbalimbali za Serikali, Asasi za kiraia, Vyama vya 
siasa vilivyosajiliwa, Taasisi  za kidini, Vijana wenye ulemavu, Shule 
za Sekondari pamoja na Shule za msingi. 






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni