WAJASIRIAMALI WAKULIMA NA WAFUGAJI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO YA MASHINE BILA DHAMANA

ab3c2a4b-b9c3-4f15-8bf3-ab71acab0bf7
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.
………………………………………………………………………………………………….
Mahmoud Ahmad Arusha
Wajasiriamali kote nchini wakiwamo pia wakulima na wafugaji nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya mikopo ya vifaa ikiwemo trekta na mashine mbali mbali za kilimo na ufugaji sambamba na
vifaa mbali mbali lengo likiwa ni kukuza kipato kwa wananchi.
Akizungumza na waanahabari meneja mikopo wa kampuni ya Wasambazaji wa vifaa kutoa mikopo kwa wajasiriamali bila dhamana yeyote (EFTA)yenye makao makuu yake Mjini Moshi mkoani Kilimanjaro Peter Temu amesema kuwa wanawakaribisha wananchi kwenye maonyesho hayo ya siku tatu yakatayofanyika mkoani hapa.
Amesema kuwa kwenye maonyesho hayo zaidi ya wauzaji na wasambazaji wa mashine 25 watakuwa wakionyesha bihdaa na mashine walizonazo kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wananchi watakaoudhuria ili wajue matumizi bora ya mashine aina,mashine halisi,waranti na mabo mengine mbali mbali bila ya kiingilio.
Alisema kuwa mbali na maonyesho hayo ya EFTA pia wamejianda kuwafanya watembeleaji wa mabanda ya maonyesho hayo kuona na kupata mambo mengi ya ziada ikiwemo kupata semina na mafunzo kwa wajasiriamali toka kwa wataalamu mbali mbali bila malipo.
“Mafunzo haya yatatolewa bure na wataalamu wenye uzoefu na masuala ya ujasiriamali na kilimo ili wakulima na wajasiriamali wapate faida ya shughili wanazofanya kama kuongeza thamani katika bidhaa wanazozalisha na vifungashio vya kilimo na viwandani”alisema Temu
Alisema hiyo itakuwa fursa muhimu nay a kipekee kwa watanzania watakaobahatika kufika kwenye viwanja vya makumbusho kwa siku tatu kuanzia Alhamisi hadi yatakapofungwa jumamosi huku wakitarajia wakazi wengi kutoka mikoa ya kaskazini ikiwemo Kilimanjaro,Tanga,Arusha na Manyara kuchangamkia na kufika kukutana na wauzaji na was am,bazaji hawa huku wakijua kuwa EFTA LTD inafanya nn kwa ajili yao katika shughuli nzima ya utoaji wa mikopo bila dhamana na kutoa huduma ya mikopo  moja kwa moja kwa wajasiriamali na wakulima wote watakaofika katika maonyesho hayo.
“Tunaposema mashine za kila Aina tunamaanisha anazohitaji mteja na sio kuwa tunamchagulia mteja,mfano mashine na vifaa vya kilimo,mashine za kufyatulia matofali,mashine za kukamulia alizeti vifaa vya maabara mashine za kutengeneza chakula cha mifugo na kutotolea vifaranga pamoja kilimo cha umwagiliaji na green house na nyingine nyingi’’Alisema Temu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni