Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.
………………………………………………………………………………………………….
Mahmoud Ahmad Arusha
Wajasiriamali kote nchini 
wakiwamo pia wakulima na wafugaji nchini wametakiwa kuchangamkia fursa 
ya mikopo ya vifaa ikiwemo trekta na mashine mbali mbali za kilimo na 
ufugaji sambamba na 
vifaa mbali mbali lengo likiwa ni kukuza kipato kwa wananchi.
vifaa mbali mbali lengo likiwa ni kukuza kipato kwa wananchi.
Akizungumza na waanahabari meneja
 mikopo wa kampuni ya Wasambazaji wa vifaa kutoa mikopo kwa 
wajasiriamali bila dhamana yeyote (EFTA)yenye makao makuu yake Mjini 
Moshi mkoani Kilimanjaro Peter Temu amesema kuwa wanawakaribisha 
wananchi kwenye maonyesho hayo ya siku tatu yakatayofanyika mkoani hapa.
Amesema kuwa kwenye maonyesho 
hayo zaidi ya wauzaji na wasambazaji wa mashine 25 watakuwa wakionyesha 
bihdaa na mashine walizonazo kutoa ushauri wa kitaalamu kwa wananchi 
watakaoudhuria ili wajue matumizi bora ya mashine aina,mashine 
halisi,waranti na mabo mengine mbali mbali bila ya kiingilio.
Alisema kuwa mbali na maonyesho 
hayo ya EFTA pia wamejianda kuwafanya watembeleaji wa mabanda ya 
maonyesho hayo kuona na kupata mambo mengi ya ziada ikiwemo kupata 
semina na mafunzo kwa wajasiriamali toka kwa wataalamu mbali mbali bila 
malipo.
“Mafunzo haya yatatolewa bure na 
wataalamu wenye uzoefu na masuala ya ujasiriamali na kilimo ili wakulima
 na wajasiriamali wapate faida ya shughili wanazofanya kama kuongeza 
thamani katika bidhaa wanazozalisha na vifungashio vya kilimo na 
viwandani”alisema Temu
Alisema hiyo itakuwa fursa muhimu
 nay a kipekee kwa watanzania watakaobahatika kufika kwenye viwanja vya 
makumbusho kwa siku tatu kuanzia Alhamisi hadi yatakapofungwa jumamosi 
huku wakitarajia wakazi wengi kutoka mikoa ya kaskazini ikiwemo 
Kilimanjaro,Tanga,Arusha na Manyara kuchangamkia na kufika kukutana na 
wauzaji na was am,bazaji hawa huku wakijua kuwa EFTA LTD inafanya nn kwa
 ajili yao katika shughuli nzima ya utoaji wa mikopo bila dhamana na 
kutoa huduma ya mikopo  moja kwa moja kwa wajasiriamali na wakulima wote
 watakaofika katika maonyesho hayo.
“Tunaposema mashine za kila Aina 
tunamaanisha anazohitaji mteja na sio kuwa tunamchagulia mteja,mfano 
mashine na vifaa vya kilimo,mashine za kufyatulia matofali,mashine za 
kukamulia alizeti vifaa vya maabara mashine za kutengeneza chakula cha 
mifugo na kutotolea vifaranga pamoja kilimo cha umwagiliaji na green 
house na nyingine nyingi’’Alisema Temu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni