Tamasha
 la Changia Damu Okoa Maisha linatarajiwa kuanza leo katika Uwanja wa 
Karume, jijini Dar es Salaam ambapo pia kutakuwa na wasanii mbalimbali.
Akizungumza
 na gazeti hili, Afisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, 
Aminiel Eligeisha alisema kuwa tamasha hilo litadumu kwa siku mbili 
kuanzia leo na kesho na kwamba watu wajitokeze kwa wingi kuchangia damu.
Vijana wa Yamoto Band wanaoongozwa na Dogo Aslay.
 
“Lengo
 la tamasha hili la Changia Damu Okoa Maisha ni kukusanya lita kati ya 
5,000 na 6,000 ambazo ni asilimia 75 ya mahitaji ya damu katika 
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,” alisema Eligeisha.
Eligeisha
 aliongeza kuwa tamasha hilo kama linavyojieleza, kwamba wachangiaji wa 
damu watakuwa wanafanya hivyo ili damu hiyo ipelekwe benki ya damu kwa 
ajili ya wagonjwa watakaoihitaji.
 
“Pia
 kutakuwepo na wasanii mbalimbali watakaotumbuiza bure wakiwemo vijana 
wa Yamoto Band wanaoongozwa na Dogo Aslay pamoja na wasanii kutoka 
nyumba ya kuibua vipaji ‘ THT’ ambao watafanya vitu vyao wakati zoezi 
hilo likiendelea,” alisema.
 
Tamasha
 hilo limedhaminiwa na Kampuni ya Global Publishers Ltd, Clouds FM, 
Pepsi Tanzania, Startimes, Abbott Fund, Benki ya CRDB, Mfuko wa Pensheni
 wa GPEF pamoja na Motisun Group Tanzania Ltd.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni