RAIS MUSEVENI AKANUSHA MADAI YA KUIBA KURA KATIKA UCHAGUZI MKUU

Rais Yoweri Museveni wa Uganda amekanusha madai ya upinzani ya wizi wa kura katika uchaguzi mkuu ulioisha, na kushutumu ukosoaji uliofanywa na Jumuiya ya Kimataifa.

Museveni alitangazwa mshindi wa urais na Tume ya Uchaguzi kwa kupata asilimia 60 ya kura, akifuatiwa na mpinzani wake mkuu, Kizza Besigye aliyepata kura asilimia 35.

Besigye medai kuibiwa kura na kutoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kutokutambua matokeo yaliyomrejesha madarakani rais Museveni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni