MANCHESTER CITY YAIFUNGA DYNAMO KIEV NYUMBANI KWAO

Manchester City imepata matokeo mazuri katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora baada ya kuifunga Dynamo Kiev kwa mabao 3-1, kwenye mchezo wao wa awali uliochezwa nchini Ukraine.

Katika mchezo huo Manchester City ilitawala katika kipindi cha kwanza na Sergio Aguero alikuwa wakwanza kutikisa nyavu za Dynamo Kiev, kabla ya David Silva naye kuongeza bao la pili.

Mchezaji wa Kiev Vitaliy Buyalsky alifunga bao kwa shuti lililopinda, lakini Yaya Toure alizima ndoto ya kurejeshwa mabao hayo kwa kupachika bao la tatu mnamo dakika ya tisini ya mchezo huo. Matokeo mengine PSV Eindhoven 0-0 Atl Madrid.
                                           David Silva akifunga bao la pili katika mchezo huo
Yaya Toure akipiga mpira wa kuzungusha uliojaa wavuni na kuandika bao la tatu la Manchester City

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni