Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi 
Bw. Ramadhan Kailima alipozindua kituo Cham mawasiliano ambapo Jumla ya 
Simu 1,381 zilipokelewa katika kituo cha Mawasiliano cha Tume ya Taifa 
ya Uchaguzi – Nec Call Center, kilichoanzishwa mahususi kwa lengo la 
kuwasaidia wapiga kura pamoja na wadau mbalimbali wa uchaguzi ili kupata
 elimu ya mpiga kura.
……………………………………………………………………………………………………………..…..
Na Lydia Churi-NEC
Hivi karibuni, Tume ya Taifa ya 
Uchaguzi kwa kushirikiana na Mradi wa ukuzaji wa Demokrasia nchini (DEP)
 chini ya shirika la Maendeleo la Kimataifa (UNDP) iliandaa mikutano ya 
tathmini ya utoaji wa Elimu ya Mpiga Kura  wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka
 jana ili kujadiliana juu ya kuboresha utoaji wa Elimu hiyo katika 
Chaguzi na kuboresha ushirikiano kati ya Tume na Wadau mbalimbali wa 
Uchaguzi.
Mikutano hiyo pia ililenga 
kuainisha maeneo ambayo wadau wanataka yafanyiwe marekebisho ili  
kuboresha utendaji kazi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika kukuza 
Demokrasia nchini na kupunguza changamoto zinazoweza kujitokeza wakati 
wa Chaguzi.
Mikutano hiyo ilifanyika kwa 
Kanda kwa kuwashirikisha Mwenyekiti wa Tume na Makamishna, Mkurugenzi wa
 Uchaguzi Wakuu wa Idara pamoja na Maafisa Kutoka Tume ya Taifa ya 
uchaguzi na Mikoa iliyoalikwa kwenye Mkutano huo.
Mikutano hii ilifanyika kuanzia 
Februari 2 hadi 11, mwaka huu katika miji ya Manyara, Arusha, 
Kilimanjaro, Tanga, Lindi, Mtwara, Mbeya, Rukwa na Katavi. Miji mingine 
ni pamoja na Pwani, Dar es Salaam, Morogoro, Unguja, Pemba, Dodoma, 
Singida, Tabora, Kigoma, Kagera, Mwanza, Geita, Shinyanga, Mara, Simiyu,
  Ruvuma, Njombe na Iringa.
Aidha, Mikutano hiyo 
ilishirikisha wadau mbalimbali wa Uchaguzi wakiwemo wawakilishi wa Asasi
 za Kiraia wa makundi mbalimbali ya jamii kama vile Wanawake, Vijana, 
Watu wenye Ulemavu, na Wazee. Wengine ni Waratibu wa Uchaguzi wa Mikoa 
(Regional Election Coordinators), Wasimamizi wa Uchaguzi wa Majimbo 
ambao pia ni Wakurugenzi wa halmashauri (Rertuning Officers), Maafisa 
Uchaguzi na Maafisa Habari kutoka kila Halmashauri ulipofanyika mkutano 
wa wadau.
Kwa mujibu wa Ibara ya 74(1) ya 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na kifungu cha 
4C cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Tume ya Taifa ya 
Uchaguzi, imepewa jukumu la kutoa Elimu ya Mpiga Kura na kusimamia 
Asasi, Makundi au watu wanaotoa Elimu hiyo. 
Kwa kuzingatia umuhimu wa jukumu 
hilo, Tume ilishirikisha Asasi za Kiraia 447 katika kuhamasisha wananchi
 na kuwaelimisha juu ya umuhimu wa kushiriki na kujitokeza kujiandikisha
 kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na pia kushiriki katika 
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Asasi za Kiraia ni wadau wakubwa 
katika mchakato wa Uchaguzi kwa kuzingatia ukweli kwamba Tume ya Taifa 
ya Uchaguzi peke yake haiwezi kuwafikia Watanzania wote kutokana na 
kutokuwa na rasilimali watu ya kutosha katika kuwafikishia Elimu ya 
Mpiga Kura pamoja na utaalamu mbalimbali wa utoaji wa Elimu hasa jinsi 
ya kuwafikia watu wenye mahitaji maalumu kama walemavu, wanawake, vijana
 pamoja na wale walioko pembezoni na maeneo yasiyofikika kwa urahisi kwa
 sababu mbalimbali zikiwemo za miundombinu
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni