NYOTA WA FILAMU WA BOLLYWOOD SANJAY DUTT ATOKA JELA

Nyota wa filamu wa Bollywood Sanjay Dutt ameachiwa huru na kutoka gerezani katika mji wa magharibi wa India wa Pune.

Dutt, 56, alifungwa kwa makosa ya kukutwa na silaha zinazohusishwa tukio la milipuko ya Mumbai la mwaka 1993 lililouwa watu 257 na kujeruhi 713.

Alitiwa hatiani kwa kununua silaha hizo kutoka kwa walipuaji, lakini alijitetea silaha hizo zilikuwa ni za kuilinda familia yake wakati wa ghasia za Wahindu Waislam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni