WATOTO WAWILI WA NCHINI AFRIKA KUSINI WAMSHTAKI TB JOSHUA

Watoto wawili raia wa Afrika Kusini wanamshtaki muhubiri maarufu barani Afrika TB Joshua kutokana na moja ya majengo yake kuanguka nchini Nigeria na kumuua baba yao mwaka 2014.

Baba huyo marehemu Kalambaie wa Kalambaie alikuwa ni miongoni mwa watu 116, waliokufa katika tukio hilo ambapo wengi walikuwa ni raia wa Afrika Kusini.

Mwaka jana 2015, mahakama Jijini Lagos ilisema kanisa hilo linapaswa kulaumiwa kwa uzembe uliopelekea jengo hilo la makazi kuanguka. TB Joshua na kanisa lake wamekuwa wakikanusha kufanya kosa lolote.
          Picha ya jengo hilo la makazi lililoanguka mwaka  2014 na kuuwa watu

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni