MASHINDANO SED MISS VALENTINE'S 2022 KUFANYIKA KESHO

Mashindano ya Sed Miss Valentine's 2022 yatafanyika kesho februari 14 mwaka 2022 Mjini Babati Mkoani Manyara huku warembo 15 wanatarajiwa kuchuana vikali kutwaa taji hilo. Afisa Masoko wa Kiwanda cha Mati Super Brand Gwandumi Mpoma ambao ndio wadhamini wakuu wa mashindano hayo wamesema kuwa wamejipanga kuhakikisha wakazi wa Babati wanafurahia mashindano hiyo amewataka wajitokeze kwa wingi. Gwandumi amesema kuwa Mashindano hayo yanalenga kuibua vipaji vya vijana na kuwapa fursa ya kufanya kazi na kiwanda hicho kupitia bidhaa mbali mbali wanazozalisha ikiwemo Strong Gin,Sed Pinepale na Tanzanite Premium Vodka. Hamisi Saidi ni Moja kati ya waandaaji wa Mashindano ya Sed Miss Valentine amesema kuwa warembo wamejiandaa vizuri katika kambi hiyo na wanatarajia ushindani utakua mkali kutokana na maandalizi waliyoyafanya. wa Upande wao washiriki wa Mashindano hayo Jenifer Paulo Mmari na Keithwin Pallangyo wamepongeza udhamini wa kampuni ya Mati Super Brands Limited kwa kuwawezesha kukaa kambini na kujiandaa vyema hivyo wamewataka wakazi Mkoa wa Manyara na Mikoa jirani kujitokeza kwa wingi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni