MAONESHO YA WIKI YA USALAMA NA AFYA KAZINI 2017 MKOANI KILIMANJARO

Maonesho ya wiki ya usalama na afya kazini yameanza leo siku ya Jumatano tarehe 26/04/2017 katika viwanja vya Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro ambapo taasisi mbalimbali za serikali na binafsi zimepata fursa ya kuonyesha namna zinavyozingatia masuala ya usalama na afya kazini kwa wafanyakazi wao.

Miongoni mwa taasisi zilizopata fursa ya kushiriki maonyesho hayo kwa mwaka huu ni pamoja na kampuni za uchimbaji wa madini za Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara ambazo zinamilikiwa na kampuni ya uchimbaji ya Acacia.

Ambapo katika maonesho hayo migodi hiyo ya imekuwa ikionesha vifaa mbalimbali vya uokozi pamoja pamoja na mbinu zitumikazo kuhakikisha mazingira ya usalama kwa wafanyakazi wao wawapo kazini.

Maadhimisho ya mwaka huu ya siku ya afya na usalama mahali pa kazi yameandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) yakiwa na kauli mbiu ya “ Ongeza wigo wa ukusanyaji na utumiaji wa takwimu za usalama na afya” .Maadhimisho hayo yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 28,2017.

Zifuatazo ni picha mbalimbali wakati wa maonesho hayo siku ya kwanza Aprili 26,2017

Banda la mgodi wa Bulyanhulu-Maafisa kutoka mgodi wa Bulyanhulu wakiandaa kupokea wageni mbalimbali
Maandalizi yanaendelea
Maafisa kutoka mgodi wa Bulyanhulu
Msaidizi wa Meneja Mkuu wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu Margaret Mandia akimkaribisha Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato akifurahia jambo baada ya kufika katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Afisa Mazingira mgodi wa Bulyanhulu Florence Nyuki akimwelezea Mkaguzi wa Mitambo Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kanda ya Kaskazini Boysafi Sabato namna mgodi huo unavyotunza mazingira na kuhakikisha usalama unakuwepo katika maeneo yao ya kazi
Afisa Mazingira mgodi wa Bulyanhulu Florence Nyuki akitoa ufafanuzi kwa mwananchi aliyefika katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Afisa uhakiki wa usalama kutoka mgodi wa Bulyanhulu Amina Mohamed akimwelezea kuhusu masuala ya usalama mgodini kwa mmoja wa wananchi waliofika katika banda hilo
Afisa Mazingira mgodi wa Bulyanhulu Florence Nyuki akitoa maelezo kwa maafisa kutoka shirika la Umeme nchini Tanzania (TANESCO) waliotembelea banda hilo
Wananchi wakiwa katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Afisa rasilimali watu mgodi wa Bulyanhulu Mwanaisha Mosha akiwaelezea watalii kuhusu DVD ya Bulyanhulu inayohusu usalama mgodini na mahusiano ya jamii
Afisa viwango vya usalama mgodi wa Bulyanhulu Setieli Kimaro akitoa elimu kuhusu mambo ya usalama mgodini kwa wananchi waliotembelea banda la la mgodi wa Bulyanhulu
Mdau kutoka Mgodi wa Williamson Diamonds Limited Gamba Isack akiangalia bango kubwa lililopo katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Wananchi wakiwa katika banda la mgodi wa Bulyanhulu
Afisa afya mgodi wa Bulyanhulu Tumaini Sylvanus akielezea kuhusu masuala ya afya mgodini
Afisa Mahusiano mgodi wa Bulyanhulu William Chungu akifurahia jambo na mwananchi aliyembelea banda la mgodi wa Bulyanhulu
Mhandisi wa uchimbaji mgodi wa Bulyanhulu Fikiri Thomas akiwaonesha wananchi namna wanavyochimba madini
Banda la mgodi wa Buzwagi- Maafisa kutoka mgodi wa Buzwagi wakijiandaa kwa ajili ya maonesho
Nje ya banda la mgodi wa Buzwagi
Mkufunzi Idara ya Uokozi mgodi wa Buzwagi Azaeli Kitange akitoa elimu kuhusu usalama mgodini kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi wa Buzwagi
Maandalizi yanaendelea
Afisa usalama na afya mgodi wa Buzwagi Mustapha Mlewa akiwaelezea wananchi kuhusu namna mgodi huo unavyojitahidi kuhakikisha wafanyakazi wake wanakuwa salama mgodini
Mwananchi akiuliza swali kwa maafisa kutoka mgodi wa Buzwagi
Mkufunzi Idara ya Uokozi mgodi wa Buzwagi Azaeli Kitange akimwonesha mwananchi aliyetembelea banda la mgodi huo vifaa vinavyotumika katika uokoaji mgodini
Afisa usalama na afya mgodi wa Buzwagi Mustapha Mlewa akitoa somo kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi wa Buzwagi
Afisa Usalama na afya mgodi wa Buzwagi Deogratius Nyantabano akimwelezea mwananchi namna mgodi huo unavyojitahidi kuhakikisha wafanyakazi wake wanakuwa salama kazini
Afisa Usalama na afya mgodi wa Buzwagi Deogratius Nyantabano akiendelea kutoa elimu kwa wananchi
Afisa Usalama na afya mgodi wa Buzwagi Deogratius Nyantabano akieleza jambo kwa mwananchi aliyetembelea banda la mgodi wa Buzwagi
Dkt. Ludovick Silima kutoka mgodi wa Buzwagi akitoa elimu ya usalama kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi huo
Dkt. Ludovick Silima kutoka mgodi wa Buzwagi akielezea masuala ya afya kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi wa Buzwagi
Wananchi wakiwa katika banda la mgodi wa Buzwagi
Banda la Mgodi wa North Mara- Maafisa kutoka mgodi wa North Mara wakijiandaa kuanza kufanya maonesho
Afisa usalama mgodi wa North Mara Samwel Nyansika akimwelezea masuala ya usalama mgodini mwananchi aliyetembelea banda hilo
Kulia ni Mratibu wa Huduma za Afya na Matibabu mgodi wa North Mara Dkt. Robert Mazengo akiwaeleza wananchi kuhusu masuala mbalimbali ya afya mgodini
Kiongozi wa awali Idara ya Mahusiano mgodi wa North Mara Annamaria Baisi akitoa somo kwa wananchi waliotembelea banda la mgodi huo
Mratibu wa Huduma za Afya na Matibabu mgodi wa North Mara Dkt. Robert Mazengo akimwonesha mwananchi kifaa kinachotumika kubaini ulevi kwa wafanyakazi wanaoweza kufika kazini huku wamelewa
Afisa usalama na afya mgodi wa North Mara Athanas Fredrick akiwaelezea masuala ya usalama mgodini wanafunzi waliotembelea banda la mgodi huo
Mwananchi akitembelea banda na mgodi wa North Mara
Mratibu wa Huduma za Afya na Matibabu mgodi wa North Mara Dkt. Robert Mazengo akitoa elimu kwa wanafunzi wa shule za msingi waliotembelea katika banda hilo
Afisa Mazingira mgodi wa North Mara Sara Cyprian akimwelezea mwanannchi namna mgodi huo unavyotunza mazingira
Afisa usalama na afya mgodi wa North Mara Alfred Mwema akitoa elimu kwa mwananchi aliyetembelea banda hilo
Mratibu wa Huduma za Afya na Matibabu mgodi wa North Mara Dkt. Robert Mazengo akimpima kilevi mmoja wa wananchi waliotembelea banda hilo wakati akiwaelezea namna wanavyopima wafanyakazi mgodini
Kiongozi Idara ya Mahusiano Jamii mgodi wa North Mara Fatuma Mssumi akielezea masuala mbalimbali kuhusu mgodi huo katika kuimarisha afya na usalama kazini.  Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

SEKTA BINAFSI YAJIPANGA KUKUTANA NA RAIS KWENYE MKUTANO WA BARAZA LA TAIFA LA BIASHARA - TNBC


WADAU wa Sekta binafsi nchini Jumanne wiki hii, wamefanya mkutano ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano wao na serikali chini ya jukwaa la Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) unaotarajiwa kufanyika Mei 6 mwaka huu.

Mkutano huo wa ndani uliandaliwa na Taasisi ya Sekta binafsi nchini - TPSF ulilenga kuwekana sawa kuhusu namna bora ya kuiwakilisha sekta binafsi katika mkutano huo muhimu, ambao Mwenyekiti wake ni Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dr. John Pombe Magufuli.

Akiwakaribisha wadau wa Sekta Binafsi katika kikao hicho cha maandalizi Mwenyekiti wa TPSF Dk. Reginald Mengi alisema Serikali na Sekta Binafsi hawakomoani, ndio maana TPSF inahimiza wafanye kazi kwa pamoja ili kulifikisha taifa kwenye uchumi wa viwanda.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Godfrey Simbeye akitoa neno la ukaribisho kwa wadau wa Sekta Binafsi kwenye mkutano wa ndani ulioambatana na chakula cha jioni kilichoandaliwa na TPSF katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi.

Dk Mengi pia alisema serikali na sekta binafsi wana malengo yanayofanana ya kutokomeza umaskini na kutengeneza ajira kwa wananchi, jambo ambalo linaweza kutekelezeka kwa urahisi iwapo kutakuwa na ushirikiano wa karibu baina ya serikali na Sekta Binafsi.

Katibu Mtendaji wa TNBC Mhandisi Raymond Mbilinyi alisema mkutano huo utakuwa ni fursa nzuri kwa serikali na sekta binafsi kubadilishana mawazo kuhusu wajibu wa kila upande katika kuboresha mazingira ya biashara na uzalishaji nchini ili kukuza uchumi wa nchi.
Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Roberto Jarrin akijitambulisha katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi akizungumza na wadau wa Sekta Binafsi katika mkutano ulioambatana na hafla ya chakula cha jioni uliofanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TBNC), Mhandisi Raymond Mbilinyi.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi akiendelea na mazungumzo na wadau wa Sekta Binafsi kwenye mkutano huo ulioambatana na chakula cha jioni katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TBNC), Mhandisi Raymond Mbilinyi akifafanua jambo katika mkutano wa ndani ambao ni sehemu ya kujiandaa kukutana na serikali chini ya Baraza la Taifa la Biashara (TBNC) linalotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi Mei jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Godfrey Simbeye wakati mkutano huo ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.

RC GAMBO AZINDUA BARABARA ARUSHA,AKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO , SAMBAMBA NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI KUSIKILIZA KERO ZAO

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gamboa akiwa ameshika mkasi ishara ya kukata utepe katika uzunduzi wa barabara ya St.James na Mahakamani leo Jijini Arusha,Kulia kwake ni mkuu wa wilaya ya Arusha mjini Gabriel Daqarro.Picha zote na Mahmoud Ahmad.

 Watoto wenye ulemavu kutoka shule ya msingi Meru wakiimba wimbo wa Taifa kama picha hapo juu inavyoonekana wakiongozwa na mwalimu Neema Lema ,na hii inayofuata hapa chini wakiongozwa na mtafsiri na mwalimu Viola Wilson .
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha akiangalia kwa makini kile ambacho mtoto mwenye ulemavu Amina kutoka shule ya msingi Meru akitumia kompyuta katika kuhariri video aliyoichagua,aliyeshika kipazasauti ni mtaalam wa masomo ya Tehama katika kitengo cha walemavu bi.Betha Denis.
 

Na.Mahmoud Ahmad,Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amtembelea na kujionea mradi wa darasa la watoto wenye ulemavu  katika shule ya msingi Meru iliyopo Jijini hapa. 

Akiwa katika shule hiyo yenye jumla ya wanafunzi 68 miongoni mwao wasichana wakiwa 34 na wavulana 28 huku walimu viziwi wakiwa wawili na mtaalam mmoja wa kitengo cha I. C. T, Gambo alijionea mwenyewe jinsi wanafunzi hao wanavyofanya kazi kwa kutumia teknolojia hiyo. 

Akisoma risala mbele ya Mkuu huyo wa mkoa  mwalimu Musa Lwambano alisema shule hiyo unajumla ya walimu 42 ambapo walimu 15 ni wa kitengo na 27 wa shule ya kawaida huku idadi ya wanafunzi ikiwa ni 1,384 wavulana wakiwa ni 709 na wasichana wakiwa ni 675

Amesema shule hiyo inawafadhili kutoka nchi ya  Finland walioshirikiana na Halmashauri ya Jiji la Arusha lililotoa Sh, milioni 20 na wafadhili wakichangia zaidi ya sh, milioni 180  huku fedha hiyo ikisaidia kujenga jengo bora la ICT na kununua vifaa kama kompyuta mpakato (laptop) 184,deskitopu 5,Projekta 6,Sola 14,Scana Kamera 4,Ipad 22, Mashine ya Laminationi na printa 4.

Pia vijana viziwi wanne wamepata ajira katika kitengo hicho hukuwakimshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia kwa kuwawezesha kupata maendeleo hayo shuleni hapo

Gambo alimpongeza walimu na wanafunzi wa shule hiyo kwa kutoa elimu kwa wanafunzi wenye ulemavu na kuwasihi walimu kuongeza juhudi za kutoa elimu kwa wanafunzi hao ili waweze kupata ajira na kujikwamua kiuchumi 

Awali Rc Gambo alijionea jinsi wanafunzi hao viziwi wakiimba wimbo wa Taifa kwa kutumia alama zao wakiongozwa na walimu wao ambao ni Veola Wilson na Neema Lema 

Gambo anaendelea na ziara yake ya siku tano Jiji hapa kwa kuzindua miradi mbalimbali ikiwemo uzinduzi wa barabara ya Mahakama na St, James uliogharimu Sh milioni 586. pamoja na kuzungumza na wananchi ili kutatua kero zao
 Gambo amewaagiza watumishi wa  jiji la Arusha wakiwemo wataalam wa vitengo mbalimbali  kuhakikisha wanatatua kero za wananchi haraka iwezekanavyo ili kuondokana na kero zinazowakabili.
 Miradi iliyokaguliwa ni pamoja   na  Visima viwili  vya maji vilivyoko magereza vilivyogharimu milioni 372, madarasa 6 Shule ya msingi Olasity,madarasa 4 ya Shule ya msingi Burka Estate ambayo yamegaharimu jumla ya  shilingi 218 milioni .

MAJALIWA AFUNGUA KONGAMANO KUHUSU MMONYOKO WA MAADILI


Z
Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya, Nchini, Rogers Siyanga akizungumza katika Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na kufunguliwa na Waziri Mkuu, kassim Majliwa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.
Z 1
  Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Alhaji Abubakary Zuberi akizungumza katika Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na kufunguliwa na Waziri Mkuu, kassim Majliwa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.
Z 2
Naibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo akizungumza katika Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na kufunguliwa na Waziri Mkuu, kassim Majliwa kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017.
Z 3
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Kongamano kuhusu Mmonyoko wa Maadili lililoandaliwa na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius, kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Aprili 24, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS DR,MAGUFULI AWASILI DODOMA KWA SHEREHE ZA MUUNGANO


unnamed
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
A
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
A 1
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
A 2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
A 3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi Abdallah Bulembo mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma.
A 4
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili mkoani Dodoma. Pembeni yake ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai.
A 5
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pamoja na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma. PICHA NA IKULU